MAFANIKIO:- Diamond na Vanessa na Taswira ya Ushindi wa Tuzo za AFRIMA 2014 Nchini Nigeria. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, December 28, 2014

MAFANIKIO:- Diamond na Vanessa na Taswira ya Ushindi wa Tuzo za AFRIMA 2014 Nchini Nigeria.

Vanessa Mdee akiwa na tuzo yake ya Best Female Artist in East Africa 2014.

  Mwanamuziki wa Tanzania Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' usiku wa kuamkia leo Desemba 28,2014, ametwaa tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Kiume Afrika Mashariki (Best Male Artist in East Africa) kutoka Tuzo za 2014 AFRIMA zilizofanyika huko jijini Lagos nchini Nigeria.

Mwanadada Vanessa Mdee yeye ameshinda tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Kike Afrika Mashariki (Best Female Artist in East Africa).

Tuzo ya Diamond imepokelewa na mwanamuziki Peter Msechu aliyekuwepo katika zoezi hilo la utoaji tuzo maana na yeye alikuwa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania tuzo hizo.
Peter Msechu akiwa amebeba tuzo kwa niaba ya Diamond Platnumz.
Peter Msechu, Vanessa Mdee na Victoria Kimani katika pozi huko Lagos, Nigeria.
UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

1 comment:

Post Bottom Ad