AFYA YANGU:-Ugonjwa wa TB hatari waingia Nchini. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, December 28, 2014

AFYA YANGU:-Ugonjwa wa TB hatari waingia Nchini.

Wakati Taifa likikabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa dawa hospitalini, aina mpya na hatari zaidi ya ugonjwa wa kifua kikuu sugu imegundulika na kuathiri mtu mmoja nchini.

 Mgonjwa huyo alibainika kuwa na kifua kikuu sugu kisicho na tiba, aina ya ‘Xtreme Drug Resistant’ au XDR-TB ambayo hapo awali haikuwa ikiwaathiri Watanzania.
Huyu ni mgonjwa wa pili kubainika kuwa na aina hii hatari ya TB baada ya kesi ya kwanza kuripotiwa mwaka 2011.

Shirika la Afya Duniani (WHO) linaeleza kuwa XDR-TB ni nadra sana ambapo ni nchi 77 tu duniani ikiwamo Tanzania zimeripoti tatizo moja moja, mwishoni mwa mwaka 2011.

Taarifa zilizokusanywa na WHO kutoka katika mataifa mbalimbali duniani zinahakiki kuwa kuna asilimia tisa tu ya kesi za XDR-TB.

MDR-TB ni kifua kikuu sugu ambacho kimeshindikana kutibika kwa dawa za mstari wa pili.

Mratibu wa Ugonjwa wa Kifua Kikuu Mkoa wa Kinondoni, Dk Hassan Lupinda alithibitisha kupokewa kwa mgonjwa huyo na kusema kuwa alipokelewa katika Hospitali ya Mwananyamala na vipimo pamoja na historia yake ilibainisha kuwa ana TB aina ya XDR.

Ni kweli tumempokea mgonjwa huyo ambaye ni Mtanzania aliyekuwa akitokea Afrika Kusini, na sasa tayari tumempeleka Kibong’oto wilayani Hai mkoani Kilimanjaro kwa matibabu,” alisema.

Wakati huohuo, takwimu za Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Nchini zinaonyesha kuwa kuna ongezeko kubwa la wagonjwa wa kifua kikuu ambapo idadi ya watu waliopimwa mwaka 2013 imeongezeka kutoka 11, 640 mwaka 2009 hadi 20,469,241 mwaka 2013.

UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

1 comment:

Post Bottom Ad