MAFANIKIO:-Taswira ya Picha ya Ujenzi wa Maabara kata ya Kabanga wilayani Ngara mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, December 27, 2014

MAFANIKIO:-Taswira ya Picha ya Ujenzi wa Maabara kata ya Kabanga wilayani Ngara mkoani Kagera.

Ujenzi wa Maabara wa Vyumba vitatu umekamilika kwa kiasi kikubwa katika shule ya Sekondari Nyabisindu iliyopo kata ya Kabanga (Pichani) wilayani Ngara mkoani Kagera hali itakayosaidia wanafunzi wa shule hiyo kusoma kwa nadharia na vitendo hasa masomo ya Sayansi kwa rahaa tupu.

 Diwani wa Kata ya Kabanga wilayani Ngara mkoani Kagera,Bw. Soud Saidr  amewapongeza Wananchi wa kata hiyo kwa Ushirikiano wao katika Ujenzi huo wa Maabara kwani katika Kata hiyo tayari ujenzi huo umekamilika kwa asilimia 100 kwa Shule ya Sekondari Kabanga na sasa Nyabisindu.

Picha hii ilipigwa Desemba 05,2014 wakati uezekaji wa bati ulipokamilika  sambamba na upigaji ripu katika Shule ya Sekondari Nyabisindu , Kata ya Kabanga wilayani Ngara mkoani Kagera.


UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad