KUPINDISHA SHERIA:- Yaliyojiri katika Picha kuhusu Ukumbi wa Bunge kuchomwa Moto huku Rais wa Burkina Faso asema atajiuzulu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, October 31, 2014

KUPINDISHA SHERIA:- Yaliyojiri katika Picha kuhusu Ukumbi wa Bunge kuchomwa Moto huku Rais wa Burkina Faso asema atajiuzulu.

Waandamanaji wakitazama ukumbi wa Bunge la Burkina Faso likiteketea kwa moto.

Waandamanaji hao wakishangilia baada ya kuchoma ukumbi wa Bunge.

Waandamanaji nchini Bukina Faso wameteketeza majengo ya Bunge mjini Ougadougou, kupinga hatua ya kuongeza muhula wa Rais Blaise Compaore ambaye ametawala nchi kwa miaka 27.

Runinga ya Kitaifa ililazimika kusitisha matangazo baada ya waandamanaji kuvamia shirika la utangazaji.

Waandamanaji kisha wameelekea Ikulu ya Rais na wanajeshi wamekua wakiwafyatulia risasi.
Rais Blaise Compaore (Pichani) wa Burkina Faso amesema atajiuzulu baada ya miezi 12 ya serikali ya mpito.

Ameyasema hayo wakati akilihutubia taifa siku moja baada ya kutokea machafuko. Wakati ambao pia Mkuu wa Majeshi wa nchi hiyo ametangaza kuivunja serikali ya nchi hiyo.

Katika hotuba yake aliyoitoa kupitia kituo binafsi cha Televisheni, Rais Compaore amesema ameuelewa ujumbe uliotolewa na waandamanaji na kwamba ataondoka madarakani baada ya kumalizika kwa kipindi cha mpito cha miezi miezi kumi na mbili.

Mmoja wa wabunge nchini Burkina Faso akitorokea kuokoa maisha yake.
Waandamanaji nchini Burkina Faso leo wamechoma moto bunge la nchi hiyo kupinga kupitishwa kwa katiba itakayomruhusu rais wa nchi hiyo, Blaise Compaore kuongeza muda wa kukaa madarakani.

Rais Compaore anataka kuongeza muda zaidi katika utawala wake wa miaka 27 aliyotumia kuliongoza taifa hilo.

Taarifa kutoka Mji Kuu ya nchi hiyo, Ouagadougou, zinasema kuwa ukumbi wa chama tawala na makao makuu ya chama hicho cha Congress for Democracy and Progress yamechomwa moto pia.

Bunge hilo lilitaka kubadili katiba itakayomuwezesha Compaore, aliyeingia madarakani tangu mwaka 1987 ili aweze kuiongoza tena nchi hiyo mwakani.

Kumekuwepo kampeni za wapinzani wanaomtaka rais huyo kuachia ngazi na kutogombea katika uchaguzi wa mwaka ujao.

Kabla ya kuchomwa moto bunge hilo, polisi walilipua mabomu ya machozi kuwazuia waandamanaji waliokuwa wakielekea katika jengo la bunge hilo japo takribani watu 1,500 walifanikiwa kupenya na kulichoma bunge hilo.

Waandamanaji walionekana wakichoma nyaraka na kupora baadhi ya vifaa vya kompyuta huku magari yaliyokuwa nje ya jengo hilo nayo yakichomwa moto huku wakisisitiza Rais huyo ajiuzulu mara moja.

Karibu kwenye familia ya Makonda Blog na uzipokee Picha/Habari zote kwa kutumiwa Mchana /Usiku baada tu ya kujiunga kwa kubonyeza hapa mtu wangu >>>BONYEZA HAPA.>>>Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad