Mtandao wa kijamii wa Ello
unapokea maombi 31,000 ya watumiaji wanaotaka kujiunga kila saa moja hali
ambayo inaibua ushindani mkubwa kwa mtandao wa Facebook.
Muanzilishi wa mtandao huo
Paul Budnitz ameiambia BBC kuwa wakati mtandao huo unaazishwa ulilenga watu
kuhudumia marafiki 90 tu.
Mtandao huu kwa mjibu wa muanzilishi
umeanzishwa August mwaka huu ukiwa ambapo hauna gharama yoyote kwa mtumiaji iwe
matangazo ama kulipia data.
Hata hivyo baadhi ya
watumiaji wameubatiza kwa jina la Anti-Facebook mtandao huo, wakimaanisha
kwamba ndiye mpinzani mkubwa wa Facebook.
Baadhi ya wataalam wa masuala
ya kimitandao wamekosoa mfumo wa Ello kutotoza gharama yoyote wakidai kuwa
katika siku za usoni huenda mtandao wa Ello utalazimika kutoza kiasi kidogo cha
fedha kwa watumiaji wake.
Paul Budnitz mtengenezaji wa
baiskel za kampuni ya Vermont ameiambia BBC kuwa wapo imara katika ushindani wa
kimitandao na kujigamba kuwa ana wataalamu wa kutosha kukabiliana na makampuni
pinzania.
Hata hivyo kuhusiana na
baadhi ya watu kuuiita kwa jinala bandia la anti-Facebook mtandao huo yeye amesema
wanajiendesha kama mtandao wenye mtazamo wake binafsi na si kutegemea mtazamo
wa mtandao wa Facebook.
|
No comments:
Post a Comment