PICHA / SIKU YA KIMATAIFA YA AMANI SEPTEMBA 21,2014:- Takwimu za Mauaji ya Albino zatisha Nchini Tanzania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, September 22, 2014

PICHA / SIKU YA KIMATAIFA YA AMANI SEPTEMBA 21,2014:- Takwimu za Mauaji ya Albino zatisha Nchini Tanzania.

Pichani ni baadhi wadau kutoka Taasisi mbalimbali pamoja na watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) wakiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja huku wakiwa wamebeba mabango yenye jumbe mbalimbali za kuhamasisha amani nchini na kupinga mauji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) nchini wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam jana Septemba 21,2014.

UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.

 

 Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

Meza kuu ikipoeka maandamano ya siku ya kimataifa ya amani kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam Septemba 21,2014.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Joseph Masasi akitoa neno la ukaribisho kwa mgeni rasmi Mh. Seif Rashid (wa pili kulia). Kutoka kushoto ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, Kamishna wa Ustawi wa Jamii, Bw. Dunford Makala, Balozi wa Uturuki nchini, Mh. Ali Davutoglu.

Wakati Katibu Mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon anahimiza serikali duniani kutafuta chanzo cha kukosekana kwa amani na kuongezeka kwa watu wenye misimamo mikali, wasemaji katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa amani Duniani wameitaka serikali ya Tanzania kutupia macho makali mauaji ya albino nchini.

Aidha Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), limeitaka serikali  kupitisha adhabu ya kunyongwa kwa wale wanaohusika na mauaji ya Albino.

Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Amani Kimataifa ya Albino jana Septemba 21,2014,jijini Dar es Salaam, Rais wa Chama cha Albino Tanzania (TAS),Bw. Joseph Tona, alisema kauli hiyo imetokana na ongezeko la idadi  ya mauaji dhidi yao.

Kadhalika, takwimu za kutoka mwaka 2006  zinaonyesha kuwa Albino 74 wameshauawa kikatili, huku 56 wakinusurika kifo, na kati yao 11 wameongezewa ulemavu mwingine wa kudumu.

Alisema hofu hiyo imesababisha maziko  yao kutokuwa na heshima kama wengine kutokana na baadhi ya familia kuwazika wapendwa wao kwa siri na wengine ndani ya nyumba, au kuweka zege nzito katika makaburi kuzuia ufukuaji wa miili yao.

Alisema licha ya serikali kuweka vikosi kazi katika kudhibiti mauaji hayo, bado haisaidii kitu kutokana na baadhi ya polisi na maofisa kuwa miongoni mwa vinara wa kupokea rushwa.

Kwa mujibu wa Tona, matukio zaidi ya 120 ni kesi za mauji ya albino, kati yake 11 ndiyo  yaliyofikishwa Mahakama, ambapo kati ya hizo kesi tano tu zimeweza kutolewa hukumu hadi sasa.


Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akisoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-Moon kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani duniani Septemba 21,2014, alisema ili kudumisha amani kuna mambo mengi yanatakiwa kufanyiwa kazi hasa kutambua chanzo cha migogoro inayosababisha msuguano mkubwa katika jamii na kukosekana kwa amani.

Mkurugenzi wa Shirika la Under The Same Sun, Vicky Ntetema,  aliishauri serikali kupitia vikosi kazi vilivyochukua jukumu la kuchunguza mauaji na ukatwaji wa viungo kwa albino, kutangaza matokeo kwa umma ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.

Pia, iuelezee umma matokeo ya kura za siri  zilizopigwa katika mikoa tangu mwaka 2009 hadi sasa zibainishwe wazi kwani nyingi zimeonyesha waganga wa jadi kutumiwa na na viongozi wa kubwa katika kuwania nyadhfa mbalimbali serikalini.

Kutokana na hofu hiyo, ameitaka serikali kurejea mkakati wa mwaka 2009 uliotolewa na  Waziri Mkuu Mizengo Pinda,  ili kupiga marufuku  leseni za waganga wa kienyeji na wale wa jadi.

Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Amani, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Mh. Seif Rashid, akisoma hotuba kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, alizitaka taasisi zilizopewa jukumu la kusimamia vitendo hivyo vya kikatili dhidi ya walemavu hususani albino kutekeleza majukumu waliyopewa kisheria kwa uadilifu mkubwa jamii ya Watanzania ione haki inatendeka ili kudumisha amani ya nchi.

Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini Tanzania (THBUB), Bi. Mary Massay akitoa nasaha kutoka kwa Tume hiyo, ambapo alitoa rai kwa mtu yeyote yule ambaye ana malalamiko au matatizo katika Haki za Binadamu anakaribishwa kwenye tume hiyo kwa ajili kupata msaada wa kisheria.

Akitoa ushuhuda mmoja kati ya waathirika ambaye mikono yake miwili imekatwa, Mariam Stanford, mkazi wa Ngara, mkoani Kagera, aliwataka wauaji wa albino wanyongwe hadharani  ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo.

“Japokuwa Tanzania inasifika ndani na nje kama kisiwa cha amani, tafsiri hiyo ni kinyume kwani ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa mauaji ya kikatili, hivyo mwito wangu kwa viongozi wa dini tumieni midomo yenu kupinga hali hii kwa sababu na sisi tumeumbwa na Mungu na tunastahili kuisha kama wengine,” alisema Miriam.

Shuhuda aliyenusurika kwenye mauaji ya Albino ambaye amekatwa mikono yote miwili, Mariam Stanford akitoa ushuhuda wake na killio chake mbele ya meza na wageni waalikwa waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam kwenye viwanja vya Mnazi mmoja.

` Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la UNDER THE SAME SUN, Vicky Ntetema akimfariji mke wa Balozi wa Uturuki nchini Yesim Davutoglu, wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani duniani iliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad