LIGI KUU UINGEREZA 2014/2015:-Hiki ndicho Manchester United ilichofanyiwa kwa kupigwa bao 5-3 huku Chelsea na Manchester City zikitoka sare. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, September 21, 2014

LIGI KUU UINGEREZA 2014/2015:-Hiki ndicho Manchester United ilichofanyiwa kwa kupigwa bao 5-3 huku Chelsea na Manchester City zikitoka sare.

Mabingwa watetezi Manchester City ikicheza mchezo wake nyumbani Etihad leo Septemba 21,2014 wa Ligi kuu Uingereza,ilifanya juhudi na kufanikiwa kulazimisha matokeo ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Chelsea.

 Andre Shuerrle aliiandikia Chelsea bao la kwanza  dakika ya 71 ya mchezo huo ,Lakini Frank Lampard akawanyima Chelsea point 3 muhimu za kujidhatiti kileleni mwa Ligi kwa kufunga bao safi la shuti kali dakika ya 85,dhidi ya Timu yake ya zamani na kipenzi Chelsea.
Zabaleta Pichani juu, ambae alilambwa Kadi ya Njano Kipindi cha Kwanza, alivaana na Diego Costa katika Dakika ya 66 na wote wawili kupewa Kadi za Njano lakini Zabaleta akatolewa nje kwa Kadi Nyekundu kwa kuwa na Kadi za Njano mbili.
Hii ni sare  ya kwanza msimu huu 2014/2015 kwa Chelsea ambayo imeshinda mechi nne mfululizo.
Nao Manchester United, wakicheza Ugenini King Power Stadium, wamechapwa Bao 5-3 katika Mechi ambayo waliongoza kwa Bao 3-1 lakini maamuzi utata ya Refa Mark Clattenburg kutoa Penati 2 kwa Leicester na ulinzi hafifu uliwapa ushindi wa chee Leicester City.

Man United walimaliza Mechi hii wakiwa Mtu 10 baada ya Beki wao Chipukizi Tyler Blackett kupewa Kadi Nyekundu Dakika ya 82 na Refa Mark Clattenburg kutoa Penati ambayo Leonardo Ulloa alifunga Bao la 5. 

Man United, wakiwa wanaongoza 3-1, Refa Clattenburg aliwapa Leicester City Penati ya ajabu baada ya Rafael kusukumwa na Vardy na Refa huyo kupeta na walipoingia ndani ya Boksi Mchezaji huyo akajiangusha na Refa huyo kutoa Penati ambayo Leicester walifunga Bao lao la Pili.

Dakika mbili baada Mkongwe Cambiasso akaisawazishia Leicester na Gemu kuwa 3-3 na kuanzia hapo kila kitu kikaenda sawa kwao na kupewa Penati nyingine.

BPL-LIGI KUU ENGLAND 2014/2015 - RATIBA:

**Saa za Bongo

Jumamosi Septemba 27,2014.

1445 Liverpool v Everton

1700 Chelsea v Aston Villa

1700 Crystal Palace v Leicester

1700 Hull v Man City

1700 Man United v West Ham

1700 Southampton v QPR

1700 Sunderland v Swansea

1930 Arsenal v Tottenham

Jumapili Septemba 28,2014.

1800 West Brom v Burnley

Jumatatu Septemba 29

2200 Stoke v Newcastle

As It Stands Table EPL 2014/2015.


Position Team Played Goal Difference Points

UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.

 Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA
No Movement 1 Chelsea 5 9 13
No Movement 2 Southampton 5 6 10
No Movement 3 Aston Villa 5 0 10
No Movement 4 Arsenal 5 4 9
No Movement 5 Swansea 5 2 9
No Movement 6 Man City 5 3 8
Moving up 7 Leicester 5 1 8
No Movement 8 West Ham 5 1 7
Moving down 9 Tottenham 5 1 7
Moving down 10 Hull 5 0 6
Moving down 11 Liverpool 5 -1 6
Moving down 12 Man Utd 5 1 5
Moving up 13 Stoke 5 -1 5
Moving down 14 Everton 5 -2 5
Moving up 15 Crystal Palace 5 -2 5
Moving up 16 West Brom 5 -4 5
Moving down 17 Sunderland 5 -1 4
Moving down 18 QPR 5 -8 4
Moving down 19 Burnley 5 -3 3
Moving down 20 Newcastle 5 -6 3

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad