Mbunge wa Mpanda Mjini, Said Arfi akiwasilisha taarifa ya kamati ya Bunge
la Katiba, bungeni mjini Dodoma Septemba 2, 2014.
|
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Waziri Mkuu, Mizengo Pindca na Naibu
Spika wa Bunge, Job Ndugai wakiteta Bungeni mjini Dodoma, Septemba 02, 2014.
|
1/. Wengine wananikejeli wanasema kwa
shughuli hii ya bunge la katiba naonyesha sifai Urais, mimi sijaomba Urais….
naifanya kazi hii kama Mwenyekiti wa bunge la katiba… basi, lakini nasema wanaochagua
ni Wananchi… inawezekana mwakani wakatamani mtu mzima alietulia, asieogopa
Wapuuzi, mtu makini, mwadilifu… kama itakua hivyo wajue tu kuna sisi wengine wa
kuweza kufikiriwa kwa mambo kama hayo.
2/. Wananchi wengi wameonyesha shauku
ya kuja kwetu hapa kinyume na ambavyo imekua ikitangazwa, makundi mbalimbali ya
Wananchi yaliyosoma rasimu yamebaini kwamba rasimu ina mapungufu kama ambavyo
sisi ndani ya kamati tumeona ina mapungufu, hili sio jambo la ajabu wala sio
kupuuza kazi iliyofanywa na tume, hapana…. tume ilifanya kazi yake vizuri.
3/. Tukumbuke kwamba Tume ilipokea
maoni kwa Wananchi zaidi ya laki 3 na mabaraza 700, walichokileta ni tafsiri
yao kuhusu maoni yao…. mnielewe vizuri hapo, na wao walikaa wakachambuuaaaaa,
mengine wakayachukua, mengine wakayakataa, mengine wakayarekebisha.
4/. Katiba tunayoitunga iwe ni katiba
ambayo itawezesha sheria zitakazokua rafiki kwa Watanzania wote.
5/. Nawasihi ndugu Wajumbe msifadhaike
na maneno ya kejeli watu wanazungumzia posho na vitu vingine, mimi mwenyekiti wenu
niko imara kabisa na kwa hulka yangu mimi hizi kejeli na matusi ni kama vile
maji kwenye mgongo wa bata, halowani…….. wengine tunaanza kuwabaini, kuna
rafiki yangu mmoja anaitwa Kubenea.
6/. Kuna Mfadhili na Wafadhili nyuma
yake wanamsogeza mbele kwa sababu wameona vipaji vyake kwa hiyo tuwaone
nao……………. kuna njia nyingi za kupata riziki tuwasamehe tu.
Like ukurasa wetu wa facebook ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA
No comments:
Post a Comment