KATIBA MPYA TANZANIA:- JUKATA Wawataja Maadui wawili wa Katiba Mpya,Wakitishia kwenda Dodoma kufunga Milango ya Bunge. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, September 13, 2014

KATIBA MPYA TANZANIA:- JUKATA Wawataja Maadui wawili wa Katiba Mpya,Wakitishia kwenda Dodoma kufunga Milango ya Bunge.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania JUKATA Deusi Kibamba akizungumza na wanahabari leo Septemba 13,2014,jijini dar es salaam juu ya mchakato huo wa katiba mpya. 

Jukwaa la katiba Tanzania (JUKATA) leo Septemba 13,2014,wamemtaja mwenyekiti wa  Bunge maalum la katiba mh SAMWELI SITTA  pamoja na mwanasheria mkuu wa serikali mh JAJI  FREDRICK WEREMA kuwa ndio maadui wapya wawili wakubwa wa mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya Tanzania.

Akizungumza na wanahabari jiji ni Dar es salaam,Mwenyekiti wa JUKATA ndugu DEUCE KIBAMBA amesema kuwa watu hao wawili watanzania waelewe kuwa ndio chanzo cha kukwama kwa mchakato huo kwa kile ambacho amekiita ni kuweka maslahi yao mbele kuliko maslahi ya watanzania kwa ujumla.

Mh KIBAMBA anasema mwenyekiti wabunge hilo mh SAMWELI SITTA  huku akijua kabisa kuwa  bunge maalum la katiba linapaswa kutoongozwa na mtu mwenye maslahi ya moja kwa moja katika serikali  aliamua kugombea katika nafasi hiyo ya uenyekiti na kukubali kuchaguliwa kwake huku akiwa ni kinara wa kushambulia vyombo vya habari,pamoja na upotoshaji mkubwa wa mchakato huo.

“Mfano mheshimiwa Sitta alitoa tamko lake kuwa hadhi ya bunge maalum la katiba ipo juu kidogo ya tume ya mabadiliko ya katiba ni upotoshaji wa makusudi wakati iko wazi kuwa vyombo hivyo viwili viko sawa kabisa, labda anataka kuonyesha kuwa yuko juu ya jaji Warioba”alisema mh Kibamba.

Aidha amesema kuwa mwenyekiti huyo mh Sitta ameamua kuendelea na bunge maalum la katiba huku akijua wazi kuwa upatikanaji wa katiba mpya haupo huku akiwa ni kinara wa kuwaaminisha watanzania kuwa katiba mpya itapatikana hata kama hakuna ushiriki wa UKAWA,wala Waziri wa katiba na sheria wa Zanzibar na Mwanasheria mkuu wa Zanzibar,ambao nao wamejitoa katika mchakato huo.

Akimzungumzia mwanasheria mkuu wa Tanzania jaji FREDRICK WEREMA amesema kuwa jaji huyo amekuwa bingwa wa kutoa tafsiri tata ambapo aliwahi kushauri kuwa tafsiri ya siku 70 ya bunge hilo ni pamoja na siku za mapumziko na sikukuu ndipo wabunge walianza kufanya kazi hadi siku za jumamosi na baadae alitoa tafsiri tofauti tena ambayo imewafanya wabunge kutofanya kazi siku za mapumziko.

“mh WEREMA amekuwa mshauri mbaya wa viongozi wa bunge hilo akiwaminisha mambo ambayo siyo, ambapo amewashauri kuwa mchakato wa katiba unaweza kukamilika bila hata ya wajumbe waliotoka nje,ndugu werema amekuwa akishauri pia muundo wa serikali tatu ulio katika rasimu unaweza kubadilika kirahisi tu jambo ambalo linapingwa na wanasheria wengi”amesema mwenyekiti wa JUKATA.

Akizungumzia maamuzi ambayo JUKUTA wamechukua kuhusu viongozi , KIBAMBA amesema kuwa viongozi hao kutokana na makosa yao wameamua kuwatangaza rasim kuwa maadui wapya wa katiba mpya ambapo wamesema kuwa wanapendekeza kuwa wasifikiriwe kupewa nafasi yoyote ya uongozi ndani ya nchi hii kwa miaka kumi  ili wapate nafasi ya kujifikiri na kujitathmini.

Aidha katika hatua nyingine JUKATA wamemtaka mwenyekiti wa bunge maalum la katiba kusitisha mara moja bunge hilo ambapo wametao wiki mbili na kama halitasitishwa wao kama JUKATA kwa wingi wao wataelekea mjini Dodoma wakiwa na makufuki kwa ajili  ya kulifunga wenyewe.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.
 
 Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad