UEFA CHAMPIONZ LIGI 2014/2015:-Haya ndio Makundi yaliyopangwa leo Agosti 28,2014 huku Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka ikienda kwa Cristiano Ronaldo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, August 28, 2014

UEFA CHAMPIONZ LIGI 2014/2015:-Haya ndio Makundi yaliyopangwa leo Agosti 28,2014 huku Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka ikienda kwa Cristiano Ronaldo.

UEFA Leo Agosti 28,2014,imempa Tuzo yao ya Mchezaji Bora wa Mwaka Cristiano Ronaldo baada ya kuwabwaga kwenye Kura Kipa wa Mabingwa wa Dunia Germany, Manuel Neuer na Mchezaji mwenzake wa Klabu ya Bayern Munich anaechezea Holland, Arjen Robben.

 Ronaldo, Miaka 29, alifunga Bao 17 katika Mechi 11 za Ulaya wakati Real Madrid inaelekea kutwaa Taji lao la 10 la Ulaya walipobeba Kombe la UEFA CHAMPIONZ LIGI na pia kuisaidia Klabu yake kutwaa Copa del Rey Msimu uliopita huko Spain.

Baada ya kukabidhiwa Tuzo yake, Ronaldo alisema: “Nimefurahi kweli kweli. Lazima niwashukuru Wachezaji wenzangu, Familia yangu, Marafiki zangu. Sina Kombe hili kwenye Makumbusho yangu, nitaliweka!

Awali Majina ya Wachezaji 35 yalipigiwa Kura na kubakia 10 na kutangazwa hapo Julai 18 na kisha kubakishwa Matatu ambayo hii Leo ndio Mshindi kapatikana.

WASHINDI WALIOPITA.

2010–2011 Lionel Messi [Barcelona]
2011–2012 Andrés Iniesta [Barcelona]
2012–2013 Franck Ribéry [Bayern Munich]

Wapigaji Kura ya Tuzo hii ni Jopo la Wanahabari maalum toka Nchi zote Wanachama wa UEFA.

Tuzo hii ilianzisha na UEFA Mwaka 2011 ili kuziba pengo la Ballon d'Or ambayo iliunganishwa na Tuzo ya FIFA ya Mchezaji Bora Duniani na pia kuibadili ile Tuzo ya zamani ya UEFA ya Mchezaji Bora wa Mwaka kwa Klabu.

LISTI YA WAGOMBEA 10.

-Diego Costa
-Angel Di Maria
-James Rodriguez
-Luis Suarez
-Philipp Lahm
-Thomas Muller
-Manuel Neuer
-Arjen Robben
-Cristiano Ronaldo
-Lionel Messi.

UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.
 
 Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA
 
Droo ya Makundi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI msimu wa mwaka 2014/2015 imefanyika huko Monaco leo Agosti 28,2014, na Makundi 8 ya Timu 4 kila moja yamepangwa ambapo kuanzia Septemba 16 Mechi zake za Mtindo wa Ligi wa Nyumbani na Ugenini zitachezwa.

Timu mbili toka kila Kundi ndizo zitasonga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 wakati Timu inayomaliza Nafasi ya 3 itatupwa EUROPA LIGI.

Kimtazamo tu Kundi gumu ni Kundi E lenye Timu za Bayern Munich, Man City, CSKA Moscow na AS Roma.

Liverpool, ambao hii ni mara yao kwanza kushiriki tangu Mwaka 2009/10, wapo Kundi B pamoja na Mabingwa Watetezi Real Madrid, FC Basel na Ludogorets.

DROO YA MAKUNDI UEFA 2014/2015.

KUNDI A.

-Atletico Madrid
-Juventus
-Olympiacos
-Malmo

KUNDI B.

-Real Madrid
-Basel
-Liverpool
-Ludogorets

KUNDI C.

-Benfica
-Zenit
-Bayer Leverkusen
-AS Monaco

KUNDI D.

-Arsenal
-Borussia Dortmund
-Galatasaray
-Anderlecht

KUNDI E.

-Bayern Munich
-Manchester City
-CSKA Moscow
-AS Roma

KUNDI F.

-FC Barcelona
-PSG
-Ajax
-Apoel

KUNDI G.

-Chelsea
-Schalke
-Sporting Lisbon
-Maribor

KUNDI H.

-FC Porto
-Shakhtar Donetsk
-Athletic Bilbao
-Bate Borisov
UEFA CHAMPIONZ LIGI 2014/2015-MPANGILIO WA MECHI/HATUA YA MAKUNDI.

MECHI-DEI
Jumanne-2014
Jumatano-2014
1
16 Septemba
17 Septemba
2
30 Septemba
01 Oktoba
3
21 Oktoba
22 Oktoba
4
4 Novemba
5 Novemba
5
25 Novemba
26 Novemba
6
9 Desemba
10 Desemba

HATUA YA MTOANO.


MECHI ZA KWANZA
MARUDIANO
Raundi ya Mtoano Timu 16
(17–18) (24–25) Februari
(10–11) (17–18) Machi
Robo Fainali
(14–15) Aprili
(21–22) Aprili
Nusu Fainali
(5–6) Mei
(12–13) Mei
Fainali
06 Juni 2015


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad