SOMA HII KUTOKA MKOANI KIGOMA:-Baada ya wawili kufa kwa Ebola Congo DRC. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, August 27, 2014

SOMA HII KUTOKA MKOANI KIGOMA:-Baada ya wawili kufa kwa Ebola Congo DRC.

WHO imesema mlipuko wa sasa wa ugonjwa wa Ebola ni wa kihistoria kutokana na kasi ya kuenea na idadi ya watu waliopoteza maisha.Mlipuko huo ambao hadi sasa umeua zaidi ya watu 1,427 Magharibi mwa Afrika.

 Juzi,Agosti 25,2014, Waziri wa Afya DRC,Bw. Felix Kabange Numbi alikaririwa akisema Ugonjwa wa Ebola umeingia nchini humo na watu wawili walioambukizwa, wamefariki dunia katika Jimbo la Ikweta, Kaskazini Magharibi wa nchi hiyo.

 Taarifa hizo zimeendelea kuwashtua na kuwafanya Majirani kuzingatia tahadhari ambapo mkuu wa mkoa wa Kigoma,Bw. Issa Machibya amesema ‘pamoja na tishio la ugonjwa huu kwamba uko DRC Congo lakini DRC ya mbali sana kule kaskazini wanakopakana na Afrika ya kati na Sudan, tumeanza kuchukua tahadhari kwenye mipaka yetu manake binadamu wanatembea na maingiliano ni makubwa’.

‘Kuanzia leo Agosti 27,2014,Bw.Machibya amesema nimemuagiza katibu tawala wa mkoa magari yote yenye uwezo wa kubeba vipaza sauti usiku au jioni watu wamesharudi nyumbani yapite kutangazia Wananchi kwa muda wa siku tatu mfululizo licha ya kuweka vipeperushi’ .

Bw.John Ndunguru ambae ni Katibu Tawala wa mkoa amesema ‘Kwenye hospitali zetu wameshatenga chumba maalum kama atatokea mgonjwa yeyote manake inabidi Wagonjwa hawa wawekewe kinga au wigo kwa siku 48, vilevile wizara ya Afya imeahidi kutuletea vifaa vya kutosha hasa vya kinga na dawa mbalimbali, tayari maafisa Afya wako hata uwanja wa ndege kukagua kila anaeingia’.

Aidha Tayari Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inatarajia kufunga vifaa vya kupimia joto (Thermal Scanner) katika mipaka ya nchi ili kudhibiti kuenea ugonjwa wa ebola ambao umeelezwa umeingia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

DRC inakuwa nchi ya tano barani Afrika kukumbwa ingawa nchi hiyo kwa mara ya kwanza ilikumbwa na ugonjwa huo mwaka 1976 kabla ya kuingia Uganda mwaka 2012. 

Nchi nyingine za Afrika zilizokumbwa na ugonjwa huo ni Liberia, Nigeria na Sierra Leone na Guinea.

UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.
 
 Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad