SOKA MULEBA:-Victoria FC yawa Bingwa wa Ligi ya Diwani wa Kata ya Kimwani wilayani Muleba mkoani Kagera- Muliga CUP 2014. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, August 02, 2014

SOKA MULEBA:-Victoria FC yawa Bingwa wa Ligi ya Diwani wa Kata ya Kimwani wilayani Muleba mkoani Kagera- Muliga CUP 2014.


Vijana wakionesha mbwembwe juzi kwenye fainali ya kombe la Muliga kata ya Kimwani wilayani Muleba,mkoani Kagera ambao ni Samweli Kalaka  (kushoto) na Barnabas Emanuel (kulia) wote wakazi wa Kyota.Habari/Picha Na:-Shaaban Ndyamukama.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.
Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA



Picha juu na chini ni Diwani wa Kata ya Kimwani wilayani Muleba mkoani Kagera  Faustini Muliga (kushoto) akikabidhi fedha na kombe lake kwa viongozi wa Timu ya Victoria FC  iliyoilaza Super Lindanda bao 4-3 kwenye ligi ya diwani huyo.



HATIMAYE kombe la Muliga katika kata ya Kimwani wilayani Muleba mkoani Kagera imefikia tamani baada ya mzunguko wa ligi  ulioshirikisha timu sita za soka  kukamilika na kuchezwa hatua ya fainali  ambayo iliahirishwa wiki mbili zilizopita baada ya kuwepo  utata wa kutafuta mshindi wa tatu.

Katika kuhitimisha ligi ya kombe hilo Timu ya soka ya Viktoria  imeibuka mshindi kwa kuilaza Super Lindanda  mabao 4-3 baada ya kulazimika kuitoa kwa matuta kwani katika dakika 90  timu hizo zilitoka kwa bao 1-1.

Akihitimisha michuano hiyo mfadhili wa kombe hilo diwani wa kata ya Kimwani Faustini Muliga alisema alianzisha ligi hiyo si kwa nia ya ushawishi wa kisiasa bali alilenga kukutanisha vijana na wananchi kwa ujumla ili kuwapa burudani .

Kwenye mashindano hayo  wananchi wa kata hiyo na vijiji vya kata jirani walihudhuria mpambano wa fainali kupata burudani iliyokuwa na timu shindani zenye utani wa jadi kati ya Victoria fc na Super Lindanda.

Mjumbe  wa kamati ya ligi hiyo Denisius  Didas alitangaza zawadi mbali mbali na diwani kukabidhi zawadi hizo na kuwataka vijana kuwa na umoja ili kwa mwakani kuwepo ligi nyingine itakayowakutanisha na wenzao wa kata  ya Nyakabango . 

Mshindi wa kwanza amepata Sh.200 000 na kombe lenye thamani ya Sh 180 000, mshindi wa pili Sh 150,000 na seti ya jezi  pia mshindi wa tatu  Vijana fc wamepata Sh.100 000 huku timu yenye nidhamu KabasharoFc  ikipata Sh.20 000.

Hata hivyo mchezo huo ililalamikiwa na makocha wa timu zote kwa kumuandama mwamuzi katika mchezo huo aliyesababisha vurugu kuwepo huku jeshi la polisi wakisusia kwa aiina yake kuimarisha usalama wakati wa upigaji matuta.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad