MAAJABU:-Tazama Picha 12 za Maiti iliyozikwa miaka 700 iliyopita ikikutwa Haijaoza. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, August 23, 2014

MAAJABU:-Tazama Picha 12 za Maiti iliyozikwa miaka 700 iliyopita ikikutwa Haijaoza.


Maiti hiyo ikiwa imetolewa nje ya Jeneza.

Ama kweli ukistaajabu ya Musa, utayaona ya Firauni....Maiti ya mwanamke iliyozikwa miaka 700 iliyopita yagunduliwa China ikiwa haijaoza. 

Ipo katika hali nzuri kiasi kwamba bado ina nyusi. Inasemekana alihifadhiwa vizuri na inaonyesha alikuwa ni mtu kutoka katika familia ya ufalme.

Maiti hiyo iligunduliwa na wafanyakazi wa barabara (wakandarasi) huko China mashariki walipopewa kazi ya kupanua barabara katika mji wa Taizhou, Mkoani wa Jiangsu. 

Wakandarasi hao walitakiwa kuchimba kwenda chini kiasi cha futi 6 ili kumaliza mwinuko uliokuwa katikati ya bara bara ndipo wakakutana kitu wasichotarajia kukikuta.

Walipokuwa wakichimba walikuta kitu kigumu  na baada ya kufanya utafiti wao kidogo ndipo waligundua kuwa kulikuwa kuna kaburi alilozikwa mtu na ndipo wakawaita wataalamu ili kuchunguza zaidi, baada ya hapo wakaamua kuweka wazi juu ya tukio hilo kuwa waligundua kwamba kaburi hilo lilikuwa na umri wa miaka 700.
Tazama picha zaidi la sakata hilo hapa chini...


Mkandarasi akijaribu kuvunja zege lililozunguka sanduku lakini kabla hawajajua kuwa kuna maiti


..........Uvunjanji wa  sanduku hilo la zege ukiendelea..........


......Wakihamaki baada ya kuona kitu ndani ya sanduku......


.......Wakianza kufunua matambara yaliyo ndani ya sanduku yaliyozunguka maiti......







UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.
Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad