Daladala lenye namba za usajili T 237 BFB aina
Toyota Hiace baada ya kuparamia lori ilitokea maeneo ya Mbalizi mkoani Mbeya Agosti 29,2014.
|
Askari wa usalama wa barabarani akiwa
anatazama na kuchunguza zaidi ajali hiyo.
|
Hivi ndivyo daladala hiyo iliyokuwa ikitoka
Mwanjelwa kuja Mbalizi ilivyoharibika baada ya ajali hiyo.
|
Picha juu na Chini ni Lori lenye namba za usajili T 158 CSV
lililoparamiwa na daladala.
|
Hapa ndipo eneo ambapo ajali imetokea, askari
wa usalama barabarani wakiendelea kufuatilia ajali hiyo.
|
...........Viti vikiwa vimeharibika baada ya ajali
kutokea.............
|
Hivi ndivyo daladala hiyo iliyokuwa ikitoka
Mwanjelwa kuja Mbalizi ilivyoharibika baada ya ajali hiyo.
|
Mashuhuda wakiwa wameizunguka daladala hiyo
kushuhudia kllichotokea.
|
Baadhi ya majeruhi wakitolewa katika Hospitali
ya Ifisi kuelekea Hospitali ya Rufaa Mbeya.
|
Watu kumi wakiwemo watoto wawili
wamefariki dunia papo hapo na wengine saba wamejeruhiwa vibaya katika ajali
iliyohusisha magari mawili.
Ajali hiyo imetokea leo majira ya
saa nne asubuhi ya Agosti 29,2014, ikihusisha gari ndogo ya abiria maarufu kama daladala lenye
namba za usajili T 237 BFB aina Toyota Hiace na gari kubwa aina ya
Fuso lenye namba za usajili T 158 CSV.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali
hiyo wamesema ajali hiyo ilitokea maeneo ya Mbalizi baada ya Hiace iliyokuwa
ikitokea Mbeya mjini kuelekea Mbalizi kulivaa lori lililokuwa likiingia
barabarani.
Walisema inasemekana dereva wa Hiace
gari yake ilimshinda kutokana na kutelemka mlima mkali wa Mbalizi ingawa pia
walimtupia lawama dereva wa lori ambaye alikuwa akiingia barabarani bila
kuchukua tahadhari.
Muuguzi Mkuu wa Hospitali Teule ya
Ifisi, Mbalizi, Sikitu Mbilinyi, ambako majeruhi na marehemu walikimbizwa hapo
alithibitisha kupokea majeruhi 7 ambapo alisema kati yao ni wanawake 3 na
wanaume 4.
Alisema kati ya majeruhi hao wawili
wamepewa rufaa kwenda Hospitali ya Rufaa Mbeya kutokana na kuhitaji msaada
zaidi huku wengine wakiendelea kupatiwa msaada wa haraka ili kunusuru hali zao.
Mbilinyi aliongeza kuwa pia
wamepokea miili ya marehemu 10 wakiwemo watoto wawili na wanawake wanne na
wanaume wanne.
Hata hivyo majina ya majeruhi na
marehemu hayajaweza kupatikana mara moja kutokana na kuwa katika hali mbaya
ambapo dereva wa lori alitokomea mara baada ya tukio.
PICHA / STORI: MBEYA YETU BLOG
Like ukurasa wetu wa facebook ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA
No comments:
Post a Comment