MICHEZO YA JUMUIYA YA MADOLA 2014:- Tazama Bendera ya Tanzania ilivyomeremeta katika sherehe za ufunguzi wa huko Glasgow, Scotland. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, July 24, 2014

MICHEZO YA JUMUIYA YA MADOLA 2014:- Tazama Bendera ya Tanzania ilivyomeremeta katika sherehe za ufunguzi wa huko Glasgow, Scotland.

Jina la Tanzania linameremeta wakati wanamichezo wetu walipopita katika maandamano ya ufunguzi wa Michezo ya Jumuiya ya Madola kwenye sherehe kabambe za ufunguzi katika Uwanja wa Celtic Park jijini Glasgow, Scotland, uliobeba watazamaji 40,000 huku watu bilioni 1 wakiangalia live sherehe hizo kupitia katika TV zao. 

 Takriban  mashabiki 100,000, na wanamichezo 4,000 kutoka katika nchi 71 zitakazoshindana wapo hapo kwa michezo hiyo ambapo hii ni mara ya 20 kufanyika toka ianzishwe.

Sehemu ya wanamichezo wa Tanzania kwenye sherehe hizo za ufunguzi. Jumla ya wanariadha 9 na kocha wao waliweka kambi nchini Ethiopia ikiwa ni jitihada za Serikali za kukuza na kuendeleza Sekta ya Michezo nchini kupitia mpango wa Diplomasia ya Michezo, ambapo wanamichezo mbalimbali wameweka kambi ambao wanamichezo wengine waliweka kambi katika nchi za Uturuki, China na New Zealand.

Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha nchini Suleiman Mjaya Nyambui (T-shirt ya njano) akihamasisha vijana wake ambapo Mbali na judo, mpira wa meza, ndondi na kuogelea, Tanzania pia inawakilishwa na timu za baiskeli na riadha.

Nahodha na bondia wa Tanzania Seleman Salum Kidunda akipeperusha juu bendera ya Taifa wakati akiongoza wenzake kwenye maandamano hayo ya ufunguzi Julai 23,2014 na Michezo hiyo ya 20 ya Jumuiya ya Madola inatarajiwa kudumu kwa siku 11 katika michezo 17 tofauti.
...........Nembo ya mashindano ya Jumuiya ya madola.................
Mashindano ya Jumuiya ya  Madola yameanza leo Julai 24,2014, mjini Glascow Scotland na kufunguliwa rasmi na Malkia Elizabeth wa Uingereza ambaye pia ni mkuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya madola.

Zaidi ya wanariadha elfu tatu wanatarajiwa kushiriki katika mashindano hayo yatakayodumu kwa muda wa majuma matatu yajayo.

Australia ndio nchi ambayo imetuma kikosi kubwa zaidi katika mashindano haya ya mwaka huu.

Takwimu rasmi zinasema kuwa Australia inaawakilishwa na zaidi ya wanariadha 400.

Mataifa yote nchi wanachama wa muungano huo kutoka kanda ya Afrika Mashariki na Kati yamewakilishwa kwenye mashindano ya mwaka huu.

Ushindani mkali unatarajiwa kuonekana katika fani mbali mbali za michezo na macho yote ya dunia , itakuwa katika shindano la riadha ambalo litatumiwa na mataifa mengi kuchagua vikosi vyao vitakavyoshiriki katika mashindano ya mabara na hatimaye kombe la dunia.

Mashindano haya yataanza rasmi hiyo leo huku wanariadha kadhaa wa Afrika Mashariki wakijibwaga ugani kuchuana na wapinzani wao katika raundi ya kwanza ya mashindano ya Judo, Masumbwi na Table tennis.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad