MAENDELEO:-Yaliyojiri Waumini wa Diini ya kiislamu wilayani Ngara mkoani Kagera walipokutana katika kata ya Mugoma kwenye baraza la Eid el Fitir-Julai 30,2014. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, July 31, 2014

MAENDELEO:-Yaliyojiri Waumini wa Diini ya kiislamu wilayani Ngara mkoani Kagera walipokutana katika kata ya Mugoma kwenye baraza la Eid el Fitir-Julai 30,2014.


Waumini  wa dini ya kiislamu wilayani Ngara mkoani Kagera Julai 30,2014,wakikutana katika kata ya Mugoma, kwenye baraza la Eid el Fitiri kujadili mambo mmbalimbali ikiwa ni pamoja na shughuli za kujiletea maendeleo kiuchumi na kijamii.


Alieshita tama ni Mkurugenzi  wa Halmashauri  ya wilaya ya  Ngara Bw Colnery Ngudungi akihudhuria baraza hilo la Eid el Fitiri na Kuwahimiza viongozi wa dini kuhamasisha waumini wa madhehebu yao kuunga mkono juhudi za ujenzi wa maabara katika shule za sekondari wilayani humo  kwani bado kuna mahitaji makubwa kwa shule hizo.

Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ngara,Bw.Hadson Bagege,Diwani wa Kata ya Mugoma,Bw.George Rubagora na kushoto kabisa ni Afisa Mtendaji wa Kata ya Mugoma,Bw.Christopher Nzoya.


Kwenye Baraza hilo mgeni rasmi alikuwa ni Shekhe wa wilaya ya Karagwe na Kyerwa  mkoani Kagera, Shekhe Nassibu  Abdul  pichani kushoto ambaye aliendesha harambee ya kuchangia fedha za kukamilisha  ujenzi wa msikiti wa Mugoma kwa gharama ya shilingi mil 30 ambapo zilipatikana sh mil 2 laki 3 ana 14,000 na mifuko 13 ya saruji.Kulia kwake ni Shekhe wa wilaya ya Ngara,Shekhe Rajab Msabaha.


Shekhe wa wilaya ya Karagwe na Kyerwa  mkoani Kagera, Shekhe Nassibu  Abdul .



Katika Baraza hilo la Eid el Fitir lilofanyika Eid pili,Julai 30,2014- Kiasi cha shilingi milioni 2 laki 7 na elfu 93 zimechangwa na waumini wa madhehebu  ya dini wakiwemo viongozi wa chama na serikali wilayani Ngara mkoani Kagera kwa ajili ya ujenzi  wa msikiti wa Mugoma wilayani Ngara.

Picha zote Na:-Shaaban Ndyamukama.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Baraza kuu la Waislamu (BAKWATA )Wilayani Ngara Bw Michael Ndyamukama  amesema kati ya fedha hizo  ambazo ni taslimu, Shilingi laki 3 na elfu 14 ni ahadi ni Shilingi milioni 2 laki 4 na elfu 80.

Bw Ndyamukama amesema  fedha hizo zimepatikana jana wakati wa baraza la idd katika harambee iliyofanyika  kata ya Mugomwa na  malengo ni kukamilisha ujenzi wa msikiti huo  ili  waumini wapate sehemu ya kufanyia ibada  kwa pamoja. 

Hata hivyo amewataka waumini kuhakikisha wanawapatia watoto wao elimu ya maadili kupitia shule za dini na elimu ya kukabiliana na changamoto za maisha kupitia mfumo wa elimu ya msingi na sekondari  kuwawezesha kuwa raia wema.

UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.

Like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad