AJALI YA BASI:-Taarifa ya Jeshi la Polisi kuhusu ajali iliyotokea asubuhi ya leo Dodoma. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, July 30, 2014

AJALI YA BASI:-Taarifa ya Jeshi la Polisi kuhusu ajali iliyotokea asubuhi ya leo Dodoma.


Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma limesema ajali iliyotokea Mapema Asubuhi leo Julai 30,2014 imesababisha vifo vya watu 17 kati yao wanaume 12, wanawake 5 na majeruhi.


Ajali hiyo imetokea majira ya saa 08:00 asubuhi eneo la Pandambili barabara ya Dodoma –Morogoro ambayo imehusisha basi la kampuni ya Moro Best yenye namba T258 AHV ambalo lilikuwa likitokea Mpwapwa kuelekea Dar es Salaam.

Basi hilo lilikuwa likiendeshwa na SAID S/O LUSOGO liligongana na Lori namba T820CKU / T390CKT lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma likiendeshwa na GILBERT S/O ISAYA NEMANYA.

Taarifa ya kamanda wa Polisi inseam katika ajali hiyo watu 17 wamepoteza maisha kati yao wanaume ni 12 na wanawake ni 5. 

Pia watu 56 wamepata majeraha mbalimbali na wamelazwa katika Hospitali za wilaya ya Kongwa na Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma. 

Miongoni mwa waliofariki ni pamoja na dereva wa lori hilo pamoja na utingo wake.

Chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa lori kutokuwa na tahadhari kwa magari yaliyokuwa yanakuja mbele yake wakati anapita (overtake) gari lingine na kwenda kuligonga busi hilo.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad