![]() |
…..Bango
hili lilikutwa wilayani Ngara mkoani Kagera katika mkutano wa UKAWA-May 24,2014
katika Viwanja vya Posta ya zamani mjini humo…
|
![]() |
UKAWA walipotinga
wilaya ya Ngara May 24,2014 wakiongozwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk. Wilbroad
Slaa.
|
![]() |
Jukwaa-uwanja
wa posta ya zamani mjini Ngara. maandalizi ya Hotuba kutoka kwa UKAWA.
|
Viongozi wa
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiwa wanaendelea kufanya mikutano ya
hadhara nchi nzima kudai Katiba ya wananchi, bado viongozi hao wanasisitiza
kwamba kamwe hawatarudi kwenye Bunge la Malaamu la Katiba kama njia za
kistaarabu za kuwaomba warudi hazitatumika.
Kabla ya
kuanza kuzunguka mikoani, Ukawa walianza kampeni za kudai Katiba inayotokana na
maoni ya wananchi kupitia Bunge Maalumu la Katiba.
Ukawa
wanapinga mchakato huo kutekwa na CCM, kwa madai kuwa wamekuwa wakitumia wingi
wao ndani ya Bunge hilo kuchakachua maoni yaliyotolewa na wananchi kupitia Tume
ya Mabadiliko ya Katiba.
Ziara za
viongozi hao wa Ukawa mikoani, zina lengo la kuunganisha nguvu za kudai Katiba
ya Wananchi na kuwashirikisha wananchi kuhusu kinachofanywa bungeni.
Vyama
vinavyounda Ukawa ambavyo viongozi wake wakuu wanazunguka mikoani ni Katibu
Mkuu wa Chadema Dk Willibrod Slaa, Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba na
Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi Mosena Nyambambe.
Baadhi ya madai
ya Ukawa yanayozungumzwa katika ziara hizo ni mwenendo wa Bunge Maalumu la
Katiba na kutekwa kwa wanasiasa kutoka chama kilicho na wajumbe wengi ndani ya
Bunge Maalumu la Katiba.
Wakati Ukawa
wakiendelea na ratiba zao za kuzunguka mikoani, Bunge Maalumu la Katiba
limesimama kwa muda hadi mwezi Agosti kupisha Bunge la Bajeti ambalo
linaendelea mjini Dodoma.
No comments:
Post a Comment