Picha Juu na Chini......Hawa ni Halmashauri ya wilaya ya Bukoba .......Mashindano ya UMISETA 2014
Ngazi ya mkoa wa Kagera...
|
...Baadhi ya Viongozi na Wakuu wa Shule za sekondali mbalimbali nao walikuwepo.....kushuhudia Vijana wao wakishindana.....
|
......Mzee Malimbu nae hakukosekana katika kuisapoti wilaya yake ya Ngara.... |
Licha ya kiwanja kuwa kibovu ,Katika mchezo wa Kikapu Halmashauri ya wilaya ya Bukoba waliibuka wababe kimkoa kwa kuwa washindi wa Kwanza,wapili Manispaa na watatu Ngara. |
Kwenye mchezo wa NETBALL ,Halmashauri ya wilaya ya Muleba iliibuka Bingwa kwa kuwafunga magoli 19 - 11 Biharamulo na Manispaa Bukoba kuibuka washindi wa tatu. |
Mkuu wa mkoa wa Kagera,Fabian Massawe akiwa ni mwana michezo hodari nae hakukosa nafasi ya kuitazama michezo ya Kikapu ,Soka na Wavu iliyokuwa ikichezwa katika viwanja hivyo vya Michezo Katoke. |
Mashindano ya UMISETA 2014
Ngazi ya mkoa wa Kagera yamefikia tamati kwa kuchezwa michezo ya fainali ili
kupata Mabingwa wa Mkoa.
Katika michezo ya fainali
,Soka Wanaume,Mabingwa wa Mkoa waliibuka Manispaa ya Bukoba kwa kuwafunga
Misenyi penati 5-4.
Halmashauri ya wilaya ya
Ngara ilifanikiwa kuibuka mshindi wa Tatu wa UMISETA 2014 Ngazi ya Mkoa wa
Kagera kwa kuwafunga wapinzani wao wa jadi Biharamulo bao 2-1 katika mchezo wa
kumtafuta mshindi wa tatu.
Aidha Mshindi wa kwanza
katika soka la Wanawake ni Manispaa Bukoba akiwanikiwa kumfunga Muleba goli 2-1
huku wa tatu akiwa ni Halmashauri ya Bukoba baada ya kumfunga Misenyi bao 1-0.
Katika Mchezo wa WAVU ama
Volleyball-Wavulana ,Halmashauri ya Wilaya ya Ngara iliibuka Bingwa wa mkoa
UMISETA 2014 kwa kuwafunga Manispaa Bukoba seti 2-0 katika mchezo wa fainali
huku ushindi wa tatu ukienda kwa Halmashauri ya wilaya ya Biharamulo.
Nao Misenyi waliibuka
Mabingwa katika mchezo huo wa WAVU kwa upande wa wasichana wakiifunga Manispaa
Bukoba seti 2-0 katika fainali huku Muleba wakishika nafasi ya tatu.
kwa Mujibu wa timu Meneja na
Afisa michezo wilaya ya Ngara , Said Salumu amesema kuwa wilaya ya Ngara pia
walifanya vyema katika mchezo wa Handball kwa kuibuka Mabingwa wa mkoa UMISETA
kwa mara ya pili mfululizo baada ya kuwatandika Biharamulo magoli 15-11 katika
mchezo wa fainali huku Manispaa Bukoba wakiambulia nafasi ya tatu-wakati upande
wa wanawake wakiibuka Biharamulo wakifuatiwa na Manispaa Bukoba na Muleba.
Kwenye mchezo wa NETBALL
,Halmashauri ya wilaya ya Muleba iliibuka Bingwa kwa kuwafunga magoli 19 - 11 Biharamulo na Manispaa Bukoba kuibuka
washindi wa tatu.
Mchezo wa RIADHA –ambao
unabeba michezo ya Mbio,Mitupo na Miruko ambapo wilaya ya Ngara imefanikiwa
kufanya vyema kwa mwaka huu tena kwa kuacha washiriki 7 ambapo Remigius John
akiibuka mshindi wa kwanza kimkoa katika mbioa za mita 1500 na 3000 mshinidi wa
pili huku Neema Venansi akiibuka mshindi wa pili kimkoa kwa wasichana katika
mbio za mita 1500 na Vitalis Petter
akifanya vyema kwa mita 800.
Katika mchezo wa Kikapu
wilaya ya Ngara iliibuka mshindi wa tatu kwa kuifunga Misenyi vikapu 30-12
ambapo Halmashauri ya wilaya ya Bukoba waliibuka wababe kimkoa kwa kuwa washindi wa Kwanza,wapili Manispaa
na watatu.
Said Salumu amesema wilaya ya Ngara kwa mwaka huu imefanikiwa
kutoa washiriki 18 kuunda kikosi cha UMISETA ngazi ya mkoa ,kitakachopambana na
Mkoa wa Geita kuanzia May 31,Mwaka huu katika Mashindano ya Kanda kati ya mkoa
wa Kagera na Mkoa wa Geita ili kupata timu ya Kanda ya ziwa Magharibi itakayoshiriki
mashindano ya UMISETA ngazi ya Taifa ya siku 11 -kuanzia June 9 ,mwaka huu.
No comments:
Post a Comment