UHALIFU:-Tazama Picha za Bibi wa Kinaijeria aliposomewa Mashitaka ya kukutwa na Madawa ya Kulevya Uwanja wa Ndege –Dar es Salaam,Tanzania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, May 28, 2014

UHALIFU:-Tazama Picha za Bibi wa Kinaijeria aliposomewa Mashitaka ya kukutwa na Madawa ya Kulevya Uwanja wa Ndege –Dar es Salaam,Tanzania.


Mtuhumiwa alipofikishwa Mahakamani hapo (May 27, 2014) ambapo MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemsomea mashtaka raia wa Nigeria, Olabisi Ibidun Cole (65) ya tuhuma za kukamatwa na madawa ya kulevya gramu 831.94 zenye thamani ya shilingi za Kitanzania milioni 37.4.


Mwendesha Mashtaka, Jackson Chidunda, alisema mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo,  Frank Mushi,  kuwa mshtakiwa anakabiliwa na tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya alipokamatwa  Mei 19, 2014, Cole akiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere alipokutwa na madawa aina ya heroin. 

Baada ya kusomewa shtaka hilo mshtakiwa hakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa upelelezi haujakamilika. 

Kesi hiyo itasomwa tena katika mahakama hiyo Juni 10 mwaka huu na mshtakiwa amerudishwa rumande.

Chanzo:- GPL

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad