SOMA:-Ratiba ya ziara ya awamu ya Kwanza ya "UKAWA’’ -TANZANIA BARA" Tarehe 14 hadi 27 MEI 2014. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, May 13, 2014

SOMA:-Ratiba ya ziara ya awamu ya Kwanza ya "UKAWA’’ -TANZANIA BARA" Tarehe 14 hadi 27 MEI 2014.


Katibu mkuu wa CHADEMA ,Dr. WILBROAD SLAA akizungumza na wanahabari mapema jana (May 12,2014) juu ya ziara yao ya nchi nzima.


Umoja wa Katiba ya Watanzania UKAWA jana(May 12,2014) umejitokeza na kutangaza rasmi ratiba yao ya kuzunguka nchi nzima kwa lengo la kutoa elimu juu ya katiba mpya na mchakato huo ulipofikia sasa.

Akizungumza na waandishi wa habari ndani ya makao makuu ya Chama cha Wananchi CUF ,katibu mkuu wa CHADEMA ,Dr. WILBROD SLAA amesema kuwa UKAWA sasa imeanza rasmi kufanya maandamano na mikutano nchi nzima kila kona ya Tanzania kwa lengo la kuwafikia wananchi na kuwaeleza ukweli kuhusu mchakato wa katiba.


Katibu mkuu wa NCCR mageuzi MOSENA NYAMBABE akizungumza ambaye ni mmoja kati ya viongozi wa UKAWA ambao watazunguka nchi nzima ,pamoja na mambo mengine kuelezea mchakato wa Katiba Mpya.

Dr. SLAA anasema kuwa kwa wale ambao wanasema kuwa UKAWA ni nguvu ya soda wanapotea, kwani muungano huo haujaja kwa bahati mbaya kwani wamejipanga kuhakikisha kuwa inawaeleza Watanzania ukweli juu ya katiba na jinsi chama cha mapinduzai CCM wanavyoupotosha umma juu ya mchakato huo.

Aidha Dr. SLAA amesema kuwa  kauli ambazo zilitolewa na viongozi wa juu wa chama cha mapinduzi CCM kuwa Tanzania haiitaji sana katiba mpya ni kauli za mtu ambaye hajafika darasani na ni kuwapotosha watanzania na kauli hizo zinatakiwa kupigwa vita sana kwani zinaupotosha umma.


JULIUS MTATIRO akizungumza katika mkutano huo.

Waandishi wa Habari kutoka Vyombo mbalimbali wakiwa wanasikiliza kwa makini mkutano huo wa UKAWA na wanahabari jana May 12,2014.

UKAWA wametangaza kufanya maandamano na mikutano kona zote za Tanzania kwa kuigawa Tanzania kwa kanda tatu ambazo ni KANDA YA KATI,KANDA YA KASKAZINI na KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI,ambapo viongozi kutoka vyama vitatu wakiwemo makatibu wakuu wote wataongoza mikutano hiyo ambayo itaanza rasmi tarehe 14 ,May ,2014.


"UKAWA INAANZA TANZANIA BARA" RATIBA YA ZIARA YA AWAMU YA KWANZA YA UKAWA, TAREHE 14 -  27 MEI 2014. 

TIMU “A”- KANDA YA KAT.

1. Mhe. Mosena Nyambabe (NCCR) – Katibu Mkuu.

2. Mhe. Ashura Mustapha (CUF)  –  Mjumbe wa Baraza Kuu. 

3. John Heche (CHADEMA)  –  Mwenyekiti wa Vijana Taifa.
  
TAREHE ENEO LA MKUTANO.

Tarehe 14/05/2014 MOROGORO MJINI.

Tarehe  16/05/2014 SHINYANGA MJINI.

Tarehe  17/05/2014 BARIADI MJINI.

Tarehe  18/05/2014 NZEGA MJINI.

Tarehe  19/05/2014 TABORA MJINI.

Tarehe  20/05/2014 URAMBO.

Tarehe  22/05/2014 NGURUKA.

Tarehe  23/05/2014 KIGOMA MJINI.

Tarehe  24/05/2014 MNANILA.

Tarehe  25/05/2014 KASULU MJINI.

Tarehe  26/05/2014 KASULU VIJIJINI.

Tarehe  27/05/2014 KIBONDO MJINI.

TIMU “B” –  KANDA YA KASKAZINI.

1. Dr Willibroad Slaa(CHADEMA)  –  Katibu Mkuu.

 2. Mhe. Mustapha Wandwi (CUF)  –  Mjumbe wa Baraza Kuu.

 3. Ahmed Msabaha (NCCR)  –  Mjumbe wa Halmashauri Kuu.

TAREHE ENEO LA MKUTANO.

Tarehe  14/05/2014 MOSHI MJINI.

Tarehe  15/05/2014 BABATI MJINI.

Tarehe  16/05/2014 ARUSHA MJINI.

Tarehe  18/05/2014 MUSOMA MJINI.

Tarehe  19/05/2014 TARIME MJINI.

Tarehe  20/05/2014 BUNDA MJINI.

Tarehe  21/05/2014 BIHARAMULO MJINI.

Tarehe  22/05/2014 BUKOBA MJINI.

Tarehe  23/05/2014 KARAGWE MJINI.

Tarehe  24/05/2014 NGARA MJINI.

Tarehe  25/05/2014 KATORO.

Tarehe  26/05/2014 GEITA MJINI.

TIMU “C” –  NYANDA ZA JUU KUSINI.

1. Prof. Ibrahim Haruna Lipumba(CUF)  –  Mwenyekiti.

 2. Mhe. Said Issa (CHADEMA)  –  Makamu Mwenyekiti Taifa.

 3. Martin Juju Danda(NCCR)  –  Mjumbe wa Halmashauri Kuu. 

TAREHE ENEO LA MKUTANO.

Tarehe  15/05/2014 IRINGA MJINI.

Tarehe  16/05/2014 MAFINGA.

Tarehe  17/05/2014 MAKAMBAKO MJINI.

Tarehe  18/05/2014 NJOMBE MJINI.

Tarehe  19/05/2014 SONGEA MJINI.

Tarehe  20/05/2014 MBINGA MJINI.

Tarehe  22/05/2014 MBEYA MJINI.

Tarehe  23/05/2014 MOMBA.

Tarehe  24/05/2014 SUMBAWANGA MJINI.

Tarehe  25/05/2014 NAMANYERE.

Tarehe  26/05/2014 KATAVI MPANDA - MULELE (MAJIMOTO).

Tarehe  27/05/2014 MPANDA MJINI.


Aidha UKAWA umewataka wananchi wa maeneo yote yaliyotajwa mjiandae na awamu ya kwanza ya ziara hii. Awamu ya  pili itaendelea mwezi Juni na ziara za wabunge walioko bungeni mtatangaziwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad