PICHA/ZIARA YA UKAWA watingisha Mkoani Kigoma - Kasulu –Leo May 28, 2014. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, May 28, 2014

PICHA/ZIARA YA UKAWA watingisha Mkoani Kigoma - Kasulu –Leo May 28, 2014.

Hatimaye mikutano ya UKAWA imeanza rasmi mkoa wa Kigoma, leo(May 28, 2014)  mkutano umefanyika  Kasulu mjini.



Umati wa Wanachama wa UKAWA na wafuasi wa Siasa wakimsikiliza mmoja wa Viongozi wa UKAWA wakati wa mkutano wa Hadhara  baada ya kupewa ruhusa ya kuendelea na Mikutano hiyo Kasulu mjini hii leo (May 28, 2014),May 29,kabla ya kuhitimisha May 31,2014 mjini Kibondo.


Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA umesema kitendo cha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanal Mstaafu Issa Machibya  kuzuia kwa Muda mikutano ya Umoja huo kimewasababishia Hasara ya Kisiasa

Mratibu wa ziara ya UKAWA kwa Mikoa ya Kanda ya Magharibi,Bw. Peterson Mushenyera akizungumza na Radio Kwizera FM,amesema kutokana na agizo la Mkuu wa Mkoa walilazimika kutofanya mikutano kwa takribani siku nne jambo ambalo ni kinyume na malengo ya ziara yao ambapo kwa kipindi walichozuiwa walikuwa wakifanya mikutano ya ndani kwa kuzungumza na Viongozi wote wa Vyama vinavyounda UKAWA,watu mashuhuri,Viongozi wa dini pamoja na watu mbalimbali wakielimishwa kuhusu rasimu ya pili ya Katiba,hoja na nia ya kuwa na Serikali 3.

Amesema baada ya kupewa ruhusa ya kuendelea na Mikutano hiyo sasa wataanzia Kasulu mjini hii leo (May 28, 2014),May 29,kabla ya kuhitimisha May 31,2014 mjini Kibondo.

Kesho May 29, 2014-UKAWA utakuwa wilayani Buhigwe katika eneo la Muyama na May 30,2014 watakua na mkutano Kigoma Mjini.

Hivi karibuni Jeshi la Polisi  lilizuia mikutano ya Hadhara ya Umoja wa Katiba ya wananchi (UKAWA) kufanya mikutano yao mkoani Kigoma  na Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kigoma alisema mikutano hiyo imepigwa marufuku kwa usalama wa viongozi wa Ukawa.

Itakumbukwa  kwamba katibu mkuu wa NCCR-Mageuzi,Bw.Mosena Nyambabe alitiwa mbaroni na Jeshi la Polisi katika kijiji cha Nguruka wilaya ya Uvinza ,mkoani humo kwa tuhuma ya kuwadhalilisha viongozi wa Kitaifa  na kuachiwa huru kwa dhamana.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad