PICHA:-Soma Bango lililoleta utata katika mkutano wa Hadhara wa UKAWA –May 24,2014- wilayani Ngara mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, May 29, 2014

PICHA:-Soma Bango lililoleta utata katika mkutano wa Hadhara wa UKAWA –May 24,2014- wilayani Ngara mkoani Kagera.

Wananchi wenye mabango wakiwa pamoja katika mkutano wa UKAWA wilayani Ngara mkoani Kagera May 24,2014 ili Dr Slaa aweze kusomwa ujumbe  wakati aliposimama kuhutubia wananchi wa Ngara mkoani Kagera.


Picha juu na chini ,Kijana Inocent John akionesha bango la kupinga serikali tatu katika mkutano wa UKAWA wilayani Ngara mkoani Kagera -Mei 24,2014.


Katika hali isiyokuwa ya kawaida katika mkutano wa UKAWA uliofanyika May 24,2014 katika Viwanja vya Posta ya zamani Mjini Ngara,Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la Inocent John alijikuta akiwa katika wakati mgumu wa kujibu hoja baada ya kuonesha bango la kupinga serikali tatu huku akiwa hajui kusoma na kuandika..Picha zote Na:-Shaban Ndyamukama-Ngara.


Hali hiyo ilijitokeza kwenye mkutano huo wakati mjumbe wa baraza kuu la CUF Bw.Mustafa Wandwi akihutubia wananchi  waliojitokeza katika mkutano huo wa UKAWA huku akiwahamasisha  kujitokeza  kupiga kura za maoni kupendekeza serikali tatu katika rasimu ya katiba mpya.

Inocent John alionesha bango lisemalo ...''Wananchi wana matatizo mengi na Serikali tatu sio suluhisho hivyo ziendelee serikali mbili ..'' lakini alipotakiwa kutetea maoni yake alianza kusua saua na kujibu mambo ambayo sio matatizo ya wananchi.

Hata hivyo Dr Wilbroard Slaa amewataka vijana kuwa makini na wanasisa wanaopinga maendeleo na haki za binadamu kwani kijana huyo alipewa bango na wanachama wa CCM ili kuvuruga  mkutano huo bila yeye kuwa na utambuzi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad