HUZUNI TASNIA YA FILAMU NCHINI:-Wasanii Bongo Muvi wamlilia ‘’Recho’’-wafanya mkutano kupanga Mazishi ...''R.IP.. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, May 28, 2014

HUZUNI TASNIA YA FILAMU NCHINI:-Wasanii Bongo Muvi wamlilia ‘’Recho’’-wafanya mkutano kupanga Mazishi ...''R.IP..


Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steve Nyerere akilia kwa uchungu kufuatia kifo cha Msanii , Rachel Haule 'Recho' aliyefariki jana (May 27,2014)saa mbili usiku katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam baada ya kujifungua ambapo mtoto wake alifariki muda mfupi na baadaye yeye akafariki.

Msanii , Rachel Haule 'Recho'enzi ya uhai wake  aliyefariki jana (May 27,2014)saa mbili usiku katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Mume wa Rachel aitwaye Saguda akiwa na majonzi.

Huzuni tele ikiwa imetawala wasanii waliokuwa viwanja ya Leaders.

 Steve akizungumza na wanachama wa Bongo Muvi, viwanja vya Leaders.

Shughuli ya kuagwa kwa mwili itafanyika kwenye viwanja vya Leaders vilivyopo Kinondoni na pia siku hiyo yatafanyika mazishi ya wote wawili yaani mama pamoja mtoto.
Taarifa ya mwanzo ya familia ilikua marehemu akazikwe kwao Songea lakini kutokana na ushawishi wa waigizaji imebidi familia ya Rachel ikubaliane na ombi lao la maziko kufanyika Dar es salaam.

MASTAA wa Bongo Muvi wamemlilia msanii mwenzao, Rachel Haule 'Recho' aliyefariki jana (May 27,2014)saa mbili usiku katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam baada ya kujifungua ambapo mtoto wake alifariki muda mfupi na baadaye yeye akafariki.

 Kwa mujibu  wa mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steve ‘Nyerere’, mwili wa Rachel utasafirishwa kwenda kwao Songea kwa ajili ya maziko. 

Taarifa zinasema Recho alikwenda Muhimbili jana kujifungua ambapo mara baada ya kujifungua mtoto alifariki na yeye hali yake kuwa mbaya, ilibidi ahamishiwe ICU ambako hali ilizidi kuwa mbaya na baadae kufariki dunia.



Shughuli ya kuagwa kwa mwili itafanyika kwenye viwanja vya Leaders vilivyopo Kinondoni na pia siku hiyo yatafanyika mazishi ya wote wawili yaani mama pamoja mtoto.

Taarifa ya mwanzo ya familia ilikua marehemu akazikwe kwao Songea lakini kutokana na ushawishi wa waigizaji imebidi familia ya Rachel ikubaliane na ombi lao la maziko kufanyika Dar es salaam.


Recho alianza rasmi kuingia katika sanaa ya maigizo mwaka 2009, katika kikundi cha Mburahati, kabla hajajiingiza rasmi kwenye uigizaji wa filamu.

Moja ya sifa zilizomfanya kujulikana, ni tabia ya kupendelea kuvaa nguo fupi, jambo ambalo alipohojiwa, alisema zinamfanya ajisikie huru na amani pindi anapofanya shughuli zake.
 
Kifo cha Recho kimekuja ndani ya wiki moja baada ya kufariki kwa msanii mwingine wa Bongo Movie ,Adam Kuambiana Jumamosi iliyopita, kifo hiki kimeleta mshtuko mkubwa kwenye tasnia ya ya filamu za kibongo. 

Mwanawamakonda Blog ...'' Inatoa pole kwa familia na wasanii wote ..''

1 comment:

  1. poleni sana kwa msiba watanzania wote na hasa wanafamilia misiba miwili kwa pamoja...Mwenyezi Mungu awape nguvu katika kipendi hiki cha huzuni.

    ReplyDelete

Post Bottom Ad