ZIARA:Kinana akagua maradi wa Maji wilayani kasulu mkoani Kigoma. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, April 09, 2014

ZIARA:Kinana akagua maradi wa Maji wilayani kasulu mkoani Kigoma.


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasabahi wananchi wa kijiji cha Nyumbigwa wilayani Kasulu,mkoani Kigoma leo (April 09,2014) walipofika na Ujumbe wake Kukagua mradi wa maji.


Mbunge wa Viti Maalum Josephine Gezabuke akizungumza na wananchi  wakati waziara ya Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana kukagua mradi wa maji wa kijiji cha Nyumbigwa .


Diwani wa Kata ya Nyumbigwa Benjamini Chalukula akiwa amebebwa juu na wananchi wa kata yake ikiwa ishara ya kuwatumikia vizuri wakati Katibu Mkuu wa CCM alipofanya ziara kwenye kata hiyo iliyopo wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma.


Tanki la maji la kijiji cha Nyumbigwa lina uwezo wa kubeba lita 290,975 na kuwahudumia zaidi ya watu elfu 11.

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Bw Abdulrahman Kinana amewataka wakazi wa wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma kuepuka Itikadi zao za kisiasa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao

Bw Kinana ametoa wito huo leo(April 09,2014)  alipokuwa akikagua ujenzi wa Mradi wa Maji unaoendelea katika Kijiji cha Nyumbigwa wilayani Kasulu katika siku ya kwanza ya ziara yake wilayani humo.

Amesema kuwa miradi yote inayojengwa kwenye vijiji vya wilaya hiyo ina lengo la kutatua changamoto zinazowasibu wakazi wa maeneo husika bila kujali itikadi ya vyama vyao vya siasa, dini, kabila wala rangi zao.

Aidha Bw Kinana ametoa kauli hiyo baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo iliyosomwa na mhandisi wa Maji wilayani humo Bw Mbaraka Rajab aliyesema kuwa mradi huo haujakamilika kwa wakati kutokana na baadhi ya wanasiasa kuingizwa masuala ya kisiasa.

Habari Na:-Radio Kwizera FM.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad