ZIARA:-Katibu mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Changamoto ya barabara wilayani Nkasi mkoani Rukwa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, April 03, 2014

ZIARA:-Katibu mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Changamoto ya barabara wilayani Nkasi mkoani Rukwa.


Ilikuwa ni shughuli nzito katika msafara wa Ndugu Kinana,barabara ni mbovu kupita maelezo kufuatia msafara huo kukumbana na changamoto ya barabara mapema jana April 01,2014, katikati ya Msitu wa hifadhi ya wilaya ya Nkasi.


  Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akimueleza jambo Mbunge wa jimbo la Nkasi Kaskazini,Mh.Ali Mohammed Kessy,walipokuwa wakitembea kwa miguu kufuatia msafara huo kukumbana na changamoto ya barabara mapema jana jioni katikati ya Msitu wa hifadhi ya wilaya ya Nkasi.

Ndugu Kinana na Msafara wake ulikuwa umetoka kijiji cha Namanyere kuelekea kijiji cha Mwampemba kusikiliza matatizo ya Wananchi na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopangwa kutekelezwa kwenye Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010.

Barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 100,lakini iliwachukua zaidi ya masaa 12 kwenda na kurudi kutokana na ubovu wa barabara.

Ndugu Kinana yuko Mkoani Rukwa,Katavi na Kigoma kwa ziara ya siku 21 ya kuimarisha Chama cha CCM,kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo kiwemo na kuzisikiliza kero mbalimbali za wananchi.


Hali ilikuwa tete mnoo,kipande cha kilometa mia kinapitika kwa zaidi ya masaa sita,kutoka kijiji kimoja kwenda kingine.

Ndugu Kinana akishiriki kuweka mawe sehemu korofi,angalau kusaidia Lori hilo pichani lililolala ndani ya msitu huo kwa siku mbili,wapite nae msafara wake uweze kuendelea na safari.

Sehemu korofi ya Barabara ikiwekwa sawa ili lori lipite na kisha msafara nao uweze kupita,lakini hata hivyo zilitumika juhudi kubwa kuvusha msafara wa Kinana na hatimae kuendelea na safari ya kuelekea kijiji kingine.

Ndugu Kinana akizungumza na baadhi ya Wanahabari aliokuwa ameambatana nao kwenye msafara wake,baada ya magari kunasa kutokana tatizo la barabara.

Pichani kulia ni Katibu Mkuu wa CCM,Ndug Kinana akiongoza kuvuka sehemu korofi ya barabara kwa miguu,huku madereva wakipiga hesabu zao namna ya kupita.

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana (alinaerusha jiwe) akishiriki kuziba sehemu korofi kwa mawe,ili msafara uweze kupita.

Mchuma ukipita sehemu korofi ya barabara kwa mbinde.

 Kila mmoja akipumua kivyake,baada ya kuvuka salama sehemu korofi ya barabara…
Picha na Michuzi Jr-Michuzi Media Group-Nkasi-RUKWA.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad