Chelsea imeanza vibaya hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa baada
ya kuchapwa mabao 3-1 na wenyeji wake PSG usiku huu April 02,2014,Katika mechi
iliyopigwa huko Ufaransa kwa wenyeji kupata bao katika dakika ya 4 tu ya mchezo
kupitia kwa Ezequiel Lavezzi, lakini Chelsea wakasawazisha katika dakika ya 27
kwa mkwaju wa penalty kupitia Eden Hazard baada ya Oscar kuangushwa.
Chelsea
walisawazisha kwa Penati ya Dakika ya 27 iliyopigwa na Eden Hazard na ilitolewa
na Refa Milorad Mazic kutoka Serbia alipoamua Sentahafu wa PSG Thiago Silva
‘kamwangusha’ Oscar.
Hadi
Mapumziko Bao zilikuwa 1-1.
PSG
walifunga Bao lao la 2 baada ya Ezequiel Lavezzi kupiga Frikiki safi ambayo
Kipa Petr Cech alishindwa kuzuia na kumparaza Zlatan Ibrahimovic kisha Mchezaji
wa Chelsea David Luiz kuusindikiza wavuni.
Nchezaji
alietoka Benchi, Javier Pastore, aliipa PSG Bao la 3 katika Dakika ya 90 baada
ya kupokea Mpira wa kurushwa na kuwatoka Cesar Azpilicueta, Frank Lampard na
John Terry kisha kupiga Shuti la chini chini na kumshinda Kipa Petr Cech.
Timu hizi
zitarudiana huko Stamford Bridge Jumanne Aprili 8.
| Oscar wa Chelsea akiangushwa na Thiago Silva wa PSG na Chelsea peneti ilitolewa na Refa Milorad Mazic kutoka Serbia . |
|
Mategemeo ya Chelsea ni katika mechi ya pili ambayo itapigwa mjini London
na ili isonge inatakiwa kushinda kuanzia mabao 2-0.
|
| Katika Dakika ya 57, Mchezaji Bora Duniani, Cristiano Ronaldo, alipiga Bao la 3 baada kumtoka Kipa Roman Weidenfeller kufuatia kupokea pasi safi ya Luka Modric. |
| Ronaldo hakumaliza Mechi hii baada ya kuumia na kutolewa nje katika Dakika ya 80 ya mchezo. |
Katika
mchezo mwingine wa Robo fainali, Real Madrid, wakicheza Uwanjan kwao Santiago
Bernabeu Jijini Madrid Nchini Hispania, Usiku wa April 02,2014,wameichapa Borussia
Dortmund Bao 3-0 katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Gareth Bale
ndie aliefunga Bao la Kwanza katika Dakika ya 3 tu baada kuunganisha pasi safi
ya Daniel Carvajal na kumzidi akili Kipa Roman Weidenfeller.
Bao la Pili
la Real lilifungwa katika Dakika ya 27 kupitia Isco kwa Shuti la chini toka
Mita 20 ambapo Katika Dakika ya 57, Mchezaji Bora Duniani, Cristiano Ronaldo,
alipiga Bao la 3 baada kumtoka Kipa Roman Weidenfeller kufuatia kupokea pasi
safi ya Luka Modric.
Hilo ni Bao
la 14 kwa Ronaldo kwenye Ligi ya
Mabingwa Msimu huu wa 2013/2014 na ameifikia Rekodi ya Lionel Messi
aliefunga Bao 14 katika Mechi 11 za UEFA Msimu wa 2011/12 wakati Ronaldo
amechukua Mechi 8 tu.
UEFA 2013/2014
ROBO FAINALI.
Marudiano
[Saa 3
Dak 45 Usiku]
[Kwenye
Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Jumanne
Aprili 8,2014.
Chelsea v Paris
Saint-Germain [1-3]
Borussia
Dortmund v Real Madrid [0-3]
Jumatano
Aprili 9,2014.
Bayern
Munich v Manchester United [1-1]
Atletico
Madrid v Barcelona [1-1]
-DROO YA
NUSU FAINALI: 11 Aprili,2014.
-Mechi
kuchezwa 22 & 23 Aprili na Marudiano 29 & 30 Aprili,2014.
-FAINALI:
Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014.






No comments:
Post a Comment