Mabingwa
watetezi wa Ligi kuu Vodacom Tanzania Bara,Yanga SC imezinduka na kufufua
matumani ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kufuatia
ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya JKT Ruvu ya Pwani, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
jioni hii.
Ushindi huo, unaifanya Yanga SC inayofundishwa na kocha Mholanzi, Hans van der Pluijm kutimiza pointi 49 baada ya kucheza mechi 23 sawa na Azam FC inayoongoza ligi hiyo kwa pointi zake 53. Mbeya City ni ya tatu kwa pointi zake 46 baada ya kucheza mechi 24.
Yanga leo(April
06,2014) ilikwenda kupumzika ikiwa inaongoza kwa mabao 3-0, Mrisho Ngassa
akifunga la kwanza dakika ya tisa akimalizia pasi nzuri ya Mrundi Didier
Kavumbangu ndani ya boksi.
Ngassa kafunga mabao 3 katika mchezo huo na kufikisha mabao 11 katika Ligi Kuu msimu huu wa 2013/2014 huku magoli mengine ya Yanga SC yamefungwa na Hussein Javu na Didier Kavumbagu nao walipiga mabao mengine mawili yaliyoiongezea Yanga akiba hiyo nzuri ya mabao hadi kufikisha matano.
Bao la kufutia machozi la JKT Ruvu inayofundishwa na kocha na mchezaji wa zamani wa Yanga SC , Freddy Felix Minziro lilifungwa na Nashon Naftali dakika ya 83 akimalizia krosi ya Damas Makwaya.
AIDHA –Kwenye
Mechi mbili pekee za Ligi Kuu Vodacom
jana April 05,2014, zilizochezwa, Kagera Sugar na Simba SC zilitoka Sare ya Bao
1-1 huko Kaitaba, Mjini Bukoba na huko Azam Complex, Chamazi, kwenye Viunga vya
Jiji la Dar es Salaam, Ashanti United ilitoka 0-0 na Mbeya City.
Ligi hiyo
itaendelea hapo April 09,2014 kwa Ruvu Shooting
kuwakaribisha Vinara wa ligi Azam FC.
Jumatano
Aprili 9,2014.
Ruvu Shooting
v Azam FC
MSIMAMO
VPL 2013/2014.
|
NA |
TIMU |
P |
W |
D |
L |
GD |
PTS |
|
1 |
Azam FC |
23 |
15 |
8 |
0 |
31 |
53 |
|
2 |
Yanga SC |
23 |
14 |
7 |
2 |
40 |
49 |
|
3 |
Mbeya City |
24 |
12 |
10 |
2 |
13 |
46 |
|
4 |
Simba SC |
24 |
9 |
10 |
5 |
15 |
37 |
|
5 |
Kagera Sugar |
23 |
8 |
10 |
5 |
3 |
34 |
|
6 |
Mtibwa Sugar |
22 |
7 |
8 |
7 |
1 |
29 |
|
7 |
Coastal Union |
23 |
6 |
11 |
6 |
0 |
29 |
|
8 |
Ruvu Shooting |
21 |
7 |
8 |
6 |
-4 |
29 |
|
9 |
JKT Ruvu |
24 |
9 |
1 |
14 |
-17 |
28 |
|
10 |
Ashanti United |
23 |
5 |
7 |
11 |
-17 |
22 |
|
11 |
Mgambo JKT |
22 |
5 |
6 |
11 |
-18 |
21 |
|
12 |
Prisons FC |
22 |
3 |
10 |
9 |
-10 |
19 |
|
13 |
JKT Oljoro |
23 |
2 |
9 |
12 |
-18 |
15 |
|
14 |
Rhino Rangers |
23 |
2 |
7 |
14 |
-19 |
13 |
**MSIMAMO HUU SI RASMI TOKA TFF






No comments:
Post a Comment