![]() |
Wachezaji wa
Simba SC wakimpongeza mfungaji wa bao lao la kuongoza, Haroun Chanongo aliyevua
jezi huku akifuta machozi ya kilio cha furaha.
|
![]() |
Picha juu na chini ni Mashabiki wa Simba SC wakishangilia timu yao jana April 19,2014 ilipocheza na Yanga SC na kutoka sare ya bao 1-1.
|
![]() |
Mfungaji wa
bao la kusawazisha la Yanga SC, Simon Msuva kushoto akishangilia na wenzake.
|
![]() |
Mashabiki wa Yanga SC wakishangilia timu yao jana April 19,2014katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam ilipocheza na Simba SC. |
![]() |
Haya ni baadhi ya Matukio yaliyojitokeza katika mchezo huo wa watani wa jadi Simba na Yanga wa kukamilisha msimu wa Ligi kuu 2013/2014 jana April 19,2014 na kutoka sare ya bao 1-1. |
![]() |
Beki wa
Simba SC, Mganda Joseph Owino kushoto akipiga kichwa dhidi ya mshambuliaji wa Yanga
SC, Didier Kavumbangu.
|
![]() |
Kocha wa
Simba SC, Mcroatia Zdravko Logarusic akitoa maelekezo kwa wachezaji wake.
|
![]() |
Kocha wa
Yanga SC, Mholanzi Hans van der Pluijm akiwatazama vijana wake.
|
![]() |
Wachezaji wa
Yanga SC baada ya kukabidhiwa Medali za ushindi wa pili Ligi Kuu iliyofikia
tamati jana (April 19,2014) kwa Azam FC kutwaa ubingwa wa ligi hiyo ya Vodacom Tanzania bara 2013/2014.
|
![]() |
Kikosi cha Yanga SC jana-April 19,2014 dhidi ya Simba SC.
|
![]() |
Kikosi cha
Simba SC jana-April 19,2014 dhidi ya Yanga SC.Picha Na:-Bin Zuberi.
|
LIGI KUU
VODACOM TANZANIA BARA 2013/2014.
Imefikia tamati (April 19,2014) kwa Mabingwa
Azam FC kukabidhiwa Kombe lao huko Azam Complex, Chamazi mara baada ya Mechi yao
ya kukamilisha Ratiba ambayo waliifunga JKT Ruvu Bao 1-0.
Kwenye
Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam, Watani wa Jadi, Yanga na Simba nao
walikutana kwenye Dabi ya Kariakoo, isiyokuwa na maana yeyote mbali ya
kukamilisha Ratiba, na kutoka Sare ya Bao 1-1.
Kwenye Mechi
hiyo, iliyohudhuriwa na Watazamaji wachache tofauti na desturi, Simba
walitangulia kufunga Bao katika Dakika ya 76 Mfungaji akiwa Haruna Chanongo na
Yanga kusawazisha kwa Bao la Dakika ya 86 la Simon Msuva.
Mechi pekee
iliyokuwa na umuhimu mkubwa ni ile iliyochezwa Uwanja wa Jamhri huko Morogoro
kati ya Tanzania Prisons na Ashanti United na Prisons kuifunga Ashanti Bao 1-0
na wao kupona na kuishusha Daraja Ashanti ambao wanaungana na JKT Oljoro na
Rhino Rangers kuporomoka Daraja.
VPL, LIGI
KUU VODACOM 2013/2014.
Mechi za
mwisho za Ligi-Jumamosi Aprili 19,2014.
Mbeya City 1
Mgambo JKT 0 [Sokoine, Mbeya]
Tanzania
Prisons 1 Ashanti United 0 [Jamhuri, Morogoro]
JKT Ruvu 0
Azam FC [Azam 1 Complex, Chamazi]
JKT Oljoro 1
Mtibwa Sugar 1 [Sheikh Amri Abeid, Arusha]
Coastal
Union 0 Kagera Sugar 1 [Mkwakwani, Tanga]
Yanga 1
Simba 1 [National Stadium, Dar es Salaam]
No comments:
Post a Comment