SHEIA:Gazeti la MAWIO Lapewa siku 3 za kujieliza kisa Hati ya Muungano. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, April 19, 2014

SHEIA:Gazeti la MAWIO Lapewa siku 3 za kujieliza kisa Hati ya Muungano.


Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene akizungumza na waandishi wa Habari April 18,2014 kuhusu Serikali kuliagiza gazeti la Mawio kueleza sababu za kupotosha na kukejeli nia njema ya serikali kwa wananchi wake kuhusu Hati ya Muungano.



Akizungumza jana (April 18,2014), Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene alisema gazeti hilo la wiki linatakiwa kujieleza ndani ya siku tatu.

Alisema mbali na kujieleza, gazeti hilo limepewa siku saba hadi Aprili 23, mwaka huu, kukanusha taarifa hiyo.


Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue ,
akiowaonesha waandishi wa habari ,
hati halisi ya Muungano ikulu jijini Dar es Salaam
(April 14,2014).
Kwa mujibu wa Mwambene, katika gazeti hilo toleo na 0091 la Aprili 17-23, mwaka huu lenye kichwa cha habari ‘Hati za Muungano utata’, taarifa husika inakebehi hati hiyo na kujenga taswira kwamba ni ya kughushi na batili.

Linadai waandishi wawili ndiyo waliona kati ya waandishi zaidi ya 20 waliokuwepo kwenye mkutano wa Katibu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.

"Taarifa ya gazeti la Mawio ni ya kimawazo na imeandikwa pasipo shaka kutimiza malengo na maslahi binafsi wanayojua,” alisema. 

Alisema pamoja na maelezo ya Katibu Kiongozi, Sefue, gazeti hilo liliamua kwa utashi wake kukejeli na kuuaminisha umma wa Watanzana kwamba Hati ya Muungano ina utata.


Hii ni sehemu ya Mkataba wa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar...1964.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad