TASWIRA:-Azam FC walivyokabidhiwa Ubingwa wao wa Kihistoria wa Ligi kuu Vodacom Tanzania bara-April 19,2014-Chamazi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, April 20, 2014

TASWIRA:-Azam FC walivyokabidhiwa Ubingwa wao wa Kihistoria wa Ligi kuu Vodacom Tanzania bara-April 19,2014-Chamazi.


Wachezaji wa Azam FC wakiongozwa na nahodha wa timu hiyo John Boko wakati wa kupokea Kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka Vodacom Tanzania Bara msimu wa mwaka 2013/2014.



Wachezaji wa Azam FC wakishangilia.


Wachezaji na mashabiki wakishangilia ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara 2013/2014.




Mashabiki wa Azam FC wakishangilia…ambapo LIGI KUU VODACOM imefikia tamati April 19,2014 kwa Mabingwa Azam FC kukabidhiwa Kombe lao huko Azam Complex, Chamazi mara baada ya Mechi yao ya kukamilisha Ratiba ambayo waliifunga JKT Ruvu Bao 1-0.


Nahodha wa Azam FC, John Boko akiwa ameshika Kombe la Ubingwa wa Ligi ya Soka Tanzania Bara-2013/2014. 

Mashabiki wa Azam FC wakishangilia…ambapo LIGI KUU VODACOM imefikia tamati April 19,2014 kwa Mabingwa Azam FC kukabidhiwa Kombe lao huko Azam Complex, Chamazi mara baada ya Mechi yao ya kukamilisha Ratiba ambayo waliifunga JKT Ruvu Bao 1-0.
Mabingwa wapya wa Tanzania Bara, Azam FC wamekabidhiwa rasmi kombe lao jana (April 19,2014)na Rais wa TFF, Jamal Malinzi.

Kombe hilo limekabidhiwa baada ya Azam FC kukipiga na JKT Ruvu na kuichapa timu hiyo ya jeshi kwa mabao 1-0 ambayo imeteremka daraja.

Bryan Umonyi, raia wa Uganda ndiye alifunga bao hilo baada ya kuingia kuchukua nafasi ya Kipre Tchetche.

Hadi wanakabidhiwa kombe, mechi hiyo ilikuwa imejaza watu wengi na mashabiki wakiwa wengi kwa kuwa pambano hilo halikuwa na kiingilio.

Lakini pia kulikuwa na shoo kutoka kwa vikundi mbalimbali wakiwemo Wanaume TMK walioongozwa na Mheshimiwa Temba.

Kikosi cha Rhino ya Tabora 2013/2014.
Aidha kumalizika kwa Ligi hiyo VPL 2013/2014-April 19,2014:-Ni rasimi sasa Rhino ya Tabora, Ashanti United na JKT Oljoro rasmi wameteremka daraja na kurejea Ligi Daraja la Kwanza.

Ashanti imeshuka baada ya kuchapwa bao 1-0 na Prisons ya Mbeya katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, April 19,2014.

Wachezaji wa Ashanti United, walilia kwa uchungu wakionyesha kutofurahia kuteremka daraja.

Rhino nao wakiwa nyumbani Tabora, jana wamepigwa mabao 2-0 na Ruvu Shooting kwa magoli ya Hamis Mohammed na Elias Maguri ndiyo yaliyoimaliza timu hiyo ya Tabora.

Kikosi cha JKT Oljoro 2013/2014.
Mjini Arusha, JKT Oljoro wameteremka rasmi baada ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Mtibwa Sugar. 

Timu hiyo ya jeshi inakuwa timu ya tatu kuteremka daraja.

Kutokana na kuteremka kwa timu hizo, Ndanda FC, Stand ya Shinyanga na Polisi ya Morogoro ndiyo wamepanda rasmi Ligi Kuu Bara msimu ujao wa 2014/2015.

Kikosi cha Ashanti United 2013/2014.
MSIMAMO WA LIGI VODACOM TANZANIA BARA 2013/2014.

NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 Azam FC 26 18 8 0 51 15 36 62
2 Young Africans 26 16 8 2 61 19 42 56
3 Mbeya City 26 13 10 3 33 20 13 49
4 Simba SC 26 9 11 6 41 27 14 38
5 Kagera Sugar 26 9 11 6 23 20 3 38
6 Ruvu Shooting 25 9 8 8 26 32 -6 35
7 Mtibwa Sugar 26 7 10 9 30 31 -1 31
8 JKT Ruvu 26 10 1 15 23 40 -17 31
9 Coastal Union 26 6 11 9 17 20 -3 29
10 Mgambo JKT 26 6 8 12 18 35 -17 26
11 Tanzania Prisons 26 6 10 10 26 33 -7 28
12 Ashanti United 26 6 7 13 20 39 -19 25
13 JKT Oljoro 26 3 10 13 19 37 -18 19
14 Rhino Rangers 25 3 7 15 18 37 -19 16

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad