UTAFITI:- Matumizi makubwa ya fedha kwa Serikali kuliko mapato inayoingiza,tatizo kwa Wananchi kuendelea kuwa masikini. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, April 29, 2014

UTAFITI:- Matumizi makubwa ya fedha kwa Serikali kuliko mapato inayoingiza,tatizo kwa Wananchi kuendelea kuwa masikini.

Imebainika kuwa uchumi wa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara umekua kutoka asilimia 4.9 mwaka jana hadi asilimia 5.5 kwa mwaka huu huku uchumi wa Tanzania ukikua kwa asilimia saba, lakini wananchi wake wakiendelea kuwa masikini.
Hayo yalibainika jana katika ripoti ya ukuaji wa Uchumi na Fedha katika ukanda wa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ya Aprili ya mwaka huu iliyowasilishwa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwa kushirikiana na Taasisi ya Tafiti za Kupunguza Umasikini (Repoa).
 
Akiiwasilisha ripoti hiyo, Mwakilishi wa IMF nchini, Thomas Baunsgaad, alisema licha ya uchumi huo kukua, lakini haujaweza kupunguza umasikini.

Alisema kwa Tanzania, gharama za mikopo kutoka nje imekuwa ni mikubwa na inaongezeka mwaka hadi mwaka na ndiyo sababu inayosabaisha hali ya umasikini kwa wananchi.

Imeeleza kuwa Tanzania kasi ya ukopaji imeongezeka  kutoka asilimia 28 ya pato la taifa hadi asilimia 42 ya pato la taifa kwa mwaka huu.

Kadhalika, ripoti hiyo imeeleza kuwa katika nchi za Afrika ili kuondokana na umasikini, lazima kuwepo na sera ambazo zitaweka kupunguza umaskini.

Baadhi ya sera hizo ni pamoja na kuhakikisha sekta ya kilimo inakuwa zaidi, kuongeza idadi ya viwanda vitakavyoongeza ajira, kuwekeza katika ukuaji na upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi, pamoja na kuboresha mazingira ya kufanya biashara.

Pia ripoti hiyo ilibaini uwapo wa matumizi makubwa ya fedha kwa serikali kuliko mapato inayoingiza.

Naye Mkurugenzi Mtendaji kutoka Repoa, Profesa Samwel Wangwe, alisema ili kupunguza hali ya umasikini nchini uendane na ukuaji wa uchumi, serikali inapaswa kupunguza matumizi makubwa ya fedha.

Source:-Nipashe.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad