UEFA 2013/2014:-Real Madrid ya Hispania na Chelsea ya England zimefanikiwa kufuzu katika hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, April 09, 2014

UEFA 2013/2014:-Real Madrid ya Hispania na Chelsea ya England zimefanikiwa kufuzu katika hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.


Demba Ba ameivusha Chelsea hadi hatua ya nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya kwa faida ya bao la ugenini baada ya sare ya jumla 3-3, usiku huu(April 08,2014)huku Chelsea ikishinda bao 2-0 ,katika mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Stamford Bridge, Jijini London.


Andre Schurrle alitangulia kuifungia Chelsea dakika ya 32, akimalizia pasi ya David Luiz na baada ya hapo PSG wakawabana The Blues hadi dakika za lala salama Ba alipofanya funga bao la Pili katika dakika za lala salama za mchezo huo.

Chelsea imeshinda kwa mabao 2-0, yakiwa yamefungwa na Andre Schurrle na Demba Ba.

Ikiwa nyumbani,Chelsea imesonga mbele kwa faida ya bao la ugenini na kuiondoa PSG ya Ufaransa baada ya  mechi ya kwanza, Chelsea ilipoteza kwa mabao 3-1, hivyo ilihitaji mabao mawili tu kusonga mbele.

Kocha Jose Mourinho ambaye timu yake ilifungwa 3-1 katika mchezo wa kwanza mjini Paris, Ufaransa alipagawa kwa furaha baada ya bao la Ba akaenda kushangilia na wachezaji wake kwenye kibendera. 


Katika mchezo mwingine wa Robo fainali, Real Madrid imefuzu kwenye tundu la sindano kwenda Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Borrusia Dortmund usiku huu(April 08,2014) Uwanja wa Signal-Iduna-Park mjini Dortmund.
Mabao ya Marco Reus dakika ya 24 na 37 yaliwafanya wenyeji waende kupumzika wanaongoza kwa 2-0 na kufanya matokeo ya jumla yawe 3-2 baada ya kufungwa 3-0 katika mchezo wa kwanza. 


CLUB ATLÉTICO DE MADRID v FC BARCELONA

-Estadio Vicente Calderon, Madrid, Nyumbani kwa Atlético Madrid, Atletico hawajawahi kuwafunga FC Barcelona tangu Februari 2010 ambapo Diego Forlán na Simão walipiga Bao na kuwapa ushindi wa Bao 2-1. 

Tangu wakati huo, Barcelona hawajafungwa katika Mechi 5 walizocheza Nyumbani kwa Atletico na mara ya mwisho kushinda ni Mei Mwaka Jana waliposhinda 2-1.

Msimu huu, Atletico na Barca zimeshakutana mara 4 na mara zote kutoka Sare lakini safari hii ni lazima Barca washinde au kupata Sare yoyote ya kuanzia Bao 2-2 ili wasonge mbele.

FC BAYERN MÜNCHEN v MANCHESTER UNITED FC 

-Allianz Arena, Munich,Bayern wanatinga kwenye Mechi hi wakiwa wameshindwa kuzifunga Klabu za England katika Mechi zao 4 zilizopita.


Wayne Rooney anena:-

Kila Mtu kila Mwaka huwa na Timu anayoona ndio itakuwa Bingwa-kama vile Barca na Bayern-lakini Siku zote halitokei hilo! Wakati Chelsea walipotwaa Ubingwa 2012, mara 3 walikaribia kutolewa! Tunaamini tutasonga! Tuna Wachezaji wazuri wa kufanya hilo!”

Bayern, ambao ni Mabingwa Watetezi wa Kombe hili, ili kusonga mbele wanahitaji Sare ya 0-0 au ushindi lakini Sare ya Bao 2-2 na kuendelea itawapa ushindi Man United kwa Bao za Ugenini.

Jumatano Aprili 9,2014.

Bayern Munich v Manchester United [1-1]

Atletico Madrid v Barcelona [1-1]

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad