SIASA:Taswira ya Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana mara baada ya kuwasili mjini Kigoma kwa ziara ya Siku tano. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, April 08, 2014

SIASA:Taswira ya Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana mara baada ya kuwasili mjini Kigoma kwa ziara ya Siku tano.


Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishuka kwenye ndege baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kigoma kuanza ziara ya siku tano mkoani humo jioni hii ya April 08,2014.


Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kigoma Dk. Walid Kaborou akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kigoma. Kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Kigoma, Mohamed Nyawenga na Katikati ya Kinana na Dk. Kaborou ni Mjumbe wa NEC Balozi Ali Karume.

Viongozi mbalimbali wa ngazi za juu za chama cha CCM Taifa na Mkoa wakiwa uwanja wa ndege mapema leo April 08,2014, jioni ,mjini Kigoma wakimsubiri kumpokea Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisindikizwa na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa Dk. Kaborou wakati akipita katika paredi la UVCCM alipopokelewa Uwanja wa Ndege wa Kigoma jioni ya leo.

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akisalimiana na Katibu wa NEC Siasa,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye,Mkuu wa mkoa wa Kigoma,Kanali Mstaafu Issa Machibya na Kamanda wa Vijana na Mchumi wa CCM mkoa wa Kigoma,Ndugu AbdulKadir Mushi mara alipowasili jioni ya leo April 08,2014,kwenye uwanja wa ndege wa Kigoma.

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Kigoma,Kanali Mstaafu Issa Machibya jioni ya leo mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kigoma.

Kinana akiondoka Uwanja wa Ndege wa Kigoma. Picha zote na Bashir Nkoromo wa CCM Blog

Sehemi ya Waendesha boda boda wakiupokea msafara wa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana mapema leo April 08,2014, jioni,mara baada ya kuwasili mjini Kigoma.


Akiwa mkoani Kigoma,Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana anaanza  ziara ya siku tano mkoani humo sambamba na ujumbe wake lengo likiwa ni kukagua uhai wa chama pamoja na kuzindua miradi kadhaa ya kimaendeleo .

Ratiba iliyotolewa na Katibu wa CCM mkoa wa Kigoma, Mohamed Nyawenga, inaonyesha kuwa, baada ya kutoka Uwanja wa Ndege, Kinana ataenda Ofisi ya CCM mkoa wa Kigoma, ambako atafanya shughuli kadhaa ikiwemo kusaini kitabu cha wageni na kupokea taarifa ya Chama, kuzungumza na Kamati ya Siasa ya mkoa na baadaye kufungua mradi wa maduka.

Ratiba hiyo inaonyesha kuwa, Aprili 9, 2014, Kinana atakwenda wilaya ya Kasulu ambako baada ya kusaini kitabu wilayani na kuzungumza katika Kikao cha Halmashauri Kuu ya wilaya hiyo, atafanya shughuli kadhaa katika Kata mbalimbali.

Kinana anaaza ziara hiyo, baada ya kumaliza nyingine ya siku sita katika mkoa wa Rukwa, ambako katika ziara hiyo alikagua uhai wa chama, utekelezaji wa ilani na Chama na kusikiliza kero za wananchi huku akijadiliana nao njia za kuzitatua pale zilizpojitokeza.

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akizungmza katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kigoma  kwenye ukumbi wa mikutano wa CCM Mkoa wa Kigoma leo-April 08,2014.

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akielezea jinsi CCM ilivyoshinda kwa kishindo katika chaguzi za Chalinze, Kalenga na madiwani wakati wa mkutano wa Halmashauri ya Mkoa wa Kigoma.
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kigoma wakisikiliza kwa makini wakati Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akizungumza nao leo-April 08,2014, baada ya kupewa taarifa ya mkoa huo.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akigalia mawe yanayotumika kujengea mabanda ya maduka yanayojengwa na CCM Mkoa wa Kigoma.
 Kinana akikagua ujenzi wa mabanda ya maduka ambao ni mradi wa CCM Mkoa wa Kigoma.
Ndugu,Kinana akiongozwa na Mchumi wa CCM Mkoa wa Kigoma, Kadri Mushi kukagua mabanda ya maduka yanayojengwa na CCM Mkoa wa Kigoma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad