 |
Balozi wa Nigeria nchini Marekani
ProfesaAdebowele Adufye, akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe Tuzo la Kiongozi Mwenye Mchango MkubwaZaidi
Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013 anayopokea kwa niabaya
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
katika sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteliya St. Regis mjini
Washington, D.C., usiku wa Jumatano, Aprili 9, 2014.
|
 |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano
waKimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe akifurahia baada ya kupokea Tuzo
laKiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika
wamwaka 2013 kwa niaba ya Rais wa Jamhuriya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa JakayaMrisho Kikwetekatika sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo
kwenye Hoteliya St. Regis mjini Washington, D.C, usiku wa jumatano,Aprili 9,
2014…Kushoto ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mhe Job Ndugai
ambaye yuko katika ziara ya kikazi ambapo naye alialikwa kuhudhuria hafla hii.
|
 |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe akimshukuru Balozi wa Nigeria nchini
Marekani Profesa Adebowele Adefuye baada ya kupokea Tuzo la Kiongozi Mwenye
Mchango Mkubwa Zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013
anayopokea kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo
kwenye Hoteli ya St. Regis mjini Washington, D.C., usiku wa , Jumatano, Aprili
9, 2014.
|
 |
Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe
LiberataMulamula akifurahia Tuzo la Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi
KatikaMaendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013 aliyopewa Rais wa Jamhuri ya
Muunganowa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika sherehe ya
kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteliya St. Regis mjini Washington, D.C., usiku wa ,
Jumatano, Aprili 9, 2014.
|
 |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe akimpa Naibu Spika Mhe Job Ndugai
Tuzo ya Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika
kwa mwaka 2013 aliyopokea kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika sherehe ya kutunuku
Tuzo hiyo kwenye Hoteli ya St. Regis mjini Washington, D.C., usiku wa ,
Jumatano, Aprili 9, 2014.
|
 |
Naibu Spika Mhe Job Ndugai ambaye yuko
Washington kwa zaiara ya kikazi akifurahia Tuzo la Kiongozi Mwenye Mchango
Mkubwa Zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013 aliyopewa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo
kwenye Hoteli ya St. Regis mjini Washington, D.C., usiku wa
, Jumatano,
Aprili 9, 2014.
|
 |
Kiongozi wa kwaya iliyotumbuiza katika hafla
hiyo akiimba atika sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteli ya St.
Regis mjini Washington, D.C., usiku wa , Jumatano, Aprili 9, 2014.
|
 |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe, akiwa na Balozi Liberata Mulamula
(kushoto) baada ya sherehe ya kupokea Tuzo la Kiongozi
Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013
aliyopokea kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika
sherehe ya
kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteli ya St. Regis mjini Washington,
D.C., usiku
wa Jumatano, Aprili 9, 2014. Picha na Ikulu.
|
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete amechaguliwa kuwa Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi katika Maendeleo
Barani Afrika kwa mwaka 2013 .
Heshima hiyo kwa Rais Kikwete imetolewa na jarida maarufu la
kimataifa la African Leadership Magazine Group na Tuzo la heshima hiyo
itatolewa jioni ya kesho, Jumatano, Aprili 9, 2014, katika sherehe
iliyopangwa kufanyika Hoteli ya St. Regis mjini Washington, D.C ikiwa ni
pamoja na chakula cha jioni.
Tuzo hiyo itapokelewa kwa niaba ya Rais Kikwete na Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe, ambaye
tayari amewasili mjini Washington kwa sherehe hiyo kubwa.
Tuzo hiyo ya heshima kubwa hutolewa kwa viongozi wa Afrika ambao
hutoa mchango mkubwa zaidi wa kiuchumi na kijamii kila mwaka kwa watu wao
na limetolewa kwa Rais Kikwete kwa mwelekeo wake usiokuwa wa kawaida na
wenye mafanikio makubwa kwa masuala ya utawala bora.
Jarida hilo linasema kuwa ukweli wa hali hiyo bora ya utawala bora
chini ya uongozi wa Rais Kikwete umeendelea kumiminiwa
sifa kimataifa na leo umeifanya Tanzania kuwa nchi ya kuigwa mfano kama
kituo cha uhakika cha uwezeshaji kutokana na mageuzi makubwa yaliyofanywa
katika sera na mifumo ya uchumi.
Jarida hilo
linasema kuwa Rais Kikwete alikuwa chaguo kubwa na la kwanza la
wasomaji wa Jarida hilo ambao walipiga kura kupitia njia mbali mbali za
mawasiliano za jarida hilo.
Linasema Jarida hilo, “Kuhusu maoni ya wasomaji wetu juu ya kiongozi
yupi wa Afrika ambaye ni hodari zaidi kwa maendeleo ya kiuchumi na
maendeleo, matokeo ya majibu ya swali hilo yamedhihirisha bila shaka yoyote
kuhusu nafasi ya Rais Kikwete katika uongozi wa nchi yake. Na ushahidi uko
kila mahali – ameweza kusimamia uchumi ambao umekuwa kwa wastani wa asili mia saba kwa miaka yote ya uongozi
wake.”
Sherehe za kesho, miongoni mwa mambo mengine, zitaliwezesha
Jarida hilo kutangaza mafanikio ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais
Kikwete kwa Jumuia ya Kimataifa, ikiwa ni pamoja na Jumuia ya Kimataifa
ya Kibiashara, wanadiplomasia na taasisi nyingine zenye ushawishi mkubwa
katika medani za kimataifa na zenye makao yake katika Jiji la Washington
na maeneo ya jirani.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
No comments:
Post a Comment