PICHA:- Rais Kikwete akabidhiwa Tuzo la Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Thursday, April 10, 2014

demo-image

PICHA:- Rais Kikwete akabidhiwa Tuzo la Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013.

.com/simgad/
TUZOYAJK1
Balozi wa Nigeria nchini Marekani ProfesaAdebowele Adufye, akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe Tuzo la Kiongozi Mwenye Mchango MkubwaZaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013 anayopokea kwa niabaya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika  sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteliya St. Regis mjini Washington, D.C., usiku wa  Jumatano, Aprili 9, 2014.

TUZO2
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano waKimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe akifurahia baada ya kupokea Tuzo laKiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika wamwaka 2013 kwa niaba ya  Rais wa Jamhuriya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa JakayaMrisho Kikwetekatika  sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteliya St. Regis mjini Washington, D.C, usiku wa jumatano,Aprili 9, 2014…Kushoto ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mhe Job Ndugai ambaye yuko katika ziara ya kikazi ambapo naye alialikwa kuhudhuria hafla hii.

TUZO3
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe akimshukuru Balozi wa Nigeria nchini Marekani Profesa Adebowele Adefuye baada ya kupokea Tuzo la Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013 anayopokea kwa niaba ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika  sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteli ya St. Regis mjini Washington, D.C., usiku wa , Jumatano, Aprili 9, 2014.

TUZO4
Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe LiberataMulamula akifurahia Tuzo la Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi KatikaMaendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013 aliyopewa Rais wa Jamhuri ya Muunganowa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika  sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteliya St. Regis mjini Washington, D.C., usiku wa , Jumatano, Aprili 9, 2014.

TUZO5
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe akimpa Naibu Spika Mhe Job Ndugai  Tuzo ya Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013 aliyopokea kwa niaba ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika  sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteli ya St. Regis mjini Washington, D.C., usiku wa , Jumatano, Aprili 9, 2014.

TUZO6
Naibu Spika Mhe Job Ndugai ambaye yuko Washington kwa zaiara ya kikazi akifurahia Tuzo la Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013 aliyopewa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika  sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteli ya St. Regis mjini Washington, D.C., usiku wa
, Jumatano, Aprili 9, 2014.

TUZO7
Kiongozi wa kwaya iliyotumbuiza katika hafla hiyo akiimba atika  sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteli ya St. Regis mjini Washington, D.C., usiku wa , Jumatano, Aprili 9, 2014.

TUZO8
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe, akiwa na Balozi Liberata Mulamula (kushoto)  baada ya sherehe  ya  kupokea  Tuzo la Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi Katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013 aliyopokea kwa niaba ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika
sherehe ya kutunuku Tuzo hiyo kwenye Hoteli ya St. Regis mjini Washington,
D.C., usiku wa Jumatano, Aprili 9, 2014. Picha na Ikulu.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amechaguliwa kuwa Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi katika Maendeleo Barani Afrika kwa mwaka 2013 .

Heshima hiyo kwa Rais Kikwete imetolewa na jarida maarufu la kimataifa la African Leadership Magazine Group na Tuzo la heshima hiyo itatolewa jioni ya kesho, Jumatano, Aprili 9, 2014, katika sherehe iliyopangwa kufanyika Hoteli ya St. Regis mjini Washington, D.C ikiwa ni pamoja na chakula cha jioni.

Tuzo hiyo itapokelewa kwa niaba ya Rais Kikwete na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe, ambaye tayari amewasili mjini Washington kwa sherehe hiyo kubwa.

Tuzo hiyo ya heshima kubwa hutolewa kwa viongozi wa Afrika ambao hutoa mchango mkubwa zaidi wa kiuchumi na kijamii kila mwaka kwa watu wao na limetolewa kwa Rais Kikwete kwa mwelekeo wake usiokuwa wa kawaida na wenye mafanikio makubwa kwa masuala ya utawala bora.

Jarida hilo linasema kuwa ukweli wa hali hiyo bora ya utawala bora chini ya  uongozi wa Rais Kikwete umeendelea kumiminiwa

sifa kimataifa na leo umeifanya Tanzania kuwa nchi ya kuigwa mfano kama kituo cha uhakika cha uwezeshaji kutokana na mageuzi makubwa yaliyofanywa katika sera na mifumo ya uchumi.

Jarida hilo linasema kuwa Rais Kikwete alikuwa chaguo kubwa na la kwanza la wasomaji wa Jarida hilo ambao walipiga kura kupitia njia mbali mbali za mawasiliano za jarida hilo.

Linasema Jarida hilo, “Kuhusu maoni ya wasomaji wetu juu ya kiongozi yupi wa Afrika ambaye ni hodari zaidi kwa maendeleo ya kiuchumi na maendeleo, matokeo ya majibu ya swali hilo yamedhihirisha bila shaka yoyote kuhusu nafasi ya Rais Kikwete katika uongozi wa nchi yake. Na ushahidi uko kila mahali – ameweza kusimamia uchumi ambao umekuwa kwa wastani wa asili mia saba kwa miaka yote ya uongozi wake.”

Sherehe za kesho, miongoni mwa mambo mengine, zitaliwezesha Jarida hilo kutangaza mafanikio ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Kikwete kwa Jumuia ya Kimataifa, ikiwa ni pamoja na Jumuia ya Kimataifa ya Kibiashara, wanadiplomasia na taasisi nyingine zenye ushawishi mkubwa katika medani za kimataifa na zenye makao yake katika Jiji la Washington na maeneo ya jirani.
         
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *