ELIMU:-Wilaya ya Biharamulo,mkoani Kagera yapanga kuwa Kidedea katika Ufaulu wa Elimu mwaka 2014. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, April 10, 2014

ELIMU:-Wilaya ya Biharamulo,mkoani Kagera yapanga kuwa Kidedea katika Ufaulu wa Elimu mwaka 2014.


Wanafunzi wa shule ya msingi Nyamigogo wilayani Biharamulo Mkoani Kagera wakiwa kwenye burudani ya kusherehekea ushindi wa kitaaluma wilayani humo jana kwenye maadhimisho ya wiki ya elimu shuleni hapo April 9,2014.


Wanafunzi hao wako umbali wa kilomita 58 kutoka biharamulo mjini makao makuu ya wilaya lakini waliweza kuonesha vituko vya burudani ambapokarika kuingia uwanjani waliandaa kasha la kukusanya tuzo kutoka kwa watazamaji.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Biharamulo na Diwani wa Kata ya Nyakahura Bw.Apolinary Mugarula akipanda miti katika shule ya msingi Nyamigogo iliyokuwa ya kwanza kiwilaya na kikata ikiwa ya 10 kimkoa na 26 kitaifa katika matokeo ya darasa la saba mwaka jana.

Mratibu Elimu Kata ya Nyamigogo Bw.Ailigi Manyesi akipanda miti katika shule ya msingi Nyamigogo iliyokuwa ya kwanza kiwilaya na kikata ikiwa ya 10 kimkoa na 26 kitaifa katika matokeo ya darasa la saba mwaka jana.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani Biharamulo mkoani Kagera, Bi.Odilia Maholelo, akipanda miti katika shule ya msingi Nyamigogo iliyokuwa ya kwanza kiwilaya na kikata ikiwa ya 10 kimkoa na 26 kitaifa katika matokeo ya darasa la saba mwaka jana.

WILAYA ya Biharamulo Mkoani Kagera ambayo katika matokeo ya ufaulu wa mitihani ya elimu ya msingi mwaka jana ilikuwa ya kwanza kimkoa na ya pili kitaifa imejipanga tena kuwa ya kwanza kwa matokeo ya kuhitimu elimu ya msingi mwaka mwaka huu.
Kaimu Afisa Elimu wilayani Biharamulo Bw. Samweli Sammy amesema hayo jana (April 9) katika maadhimisho ya wiki ya elimu yaliyofanyika katika shule ya msingi Nyamigogo iliyokuwa shule ya kwanza wilayani humo kwa matokeo ya  mwaka jana.


Kaimu Afisa Elimu wilaya,
 ya Biharamulo,mkoani kagera
Bw.Samwel Sammy.
Bw.Sammy alisema ufaulu huo utazingatiwa kwa kusimamia taaluma katika shule zote zipatazo 88 zenye wanafunzi 50711 kati yao wavulana  ni 24 966 na wasichana ni      25 745 wanaofundishwa na walimu 858 waliopo kati ya 1287 wanaohitajika.

Alisema  mikakati iliyopo katika idara hiyo ni kufanya majaribio ya mitihani ya usuli (Mock) kwa wanafunzi wa darasa la saba na la nne  ili kuwafanya wanafunzi kujenga uzoefu wa kujibu maswali ya mitihani.

Mafanikio yatapatikana kwa kutekeleza ugatuaji madaraka kwa walimu na kuwa na utawala bora kisha  kutekeleza mapendekezo ya wakaguzi ikiwa ni pamoja na kutatua kero za walimu kadri ya uwezo utakavyoruhusu”.Alisema

Aidha aliongeza kuwa mikakati mingine ni kufanya tafiti za kielimu kubaini kero ili kuzifanyia ufumbuzi kwa kulenga kufanikisha  mpango wa kitaifa wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now).

Pamoja na malengo hayo zilitajwa  baadhi ya changamoto kuwa ni upungufu wa miundombinu ya kufundishia na kujifunzia hasa vyumba vya madarasa 798 ili  kukidhi mahitaji ya vyumba  1415 kupunguza msongamano wa wanafuzi katika darasa moja.

Upungufu mwingine ni nyumba 962 za walimu kwani  walimu wanne hukaa katika nyumba moja huku  wanafuzi wakihitaji kuongezewa matundu ya vyoo 873 na  yaliyopo ni 1085 kwa wastani wanafunzi 47 hutumia tundu  moja badala ya wafafuzi 25.

Hata hivyo mgeni rasmi katika maadhimisho hayo mkuu wa wilaya ya Biharamulo Richard Mbeho  aliwashauri viongozi wa idara ya elimu na kata ya Nyamigogo wilayani humo kutobweteka na ufaulu walioupata mwaka jana kuepuka kurudi nyuma kitaaluma.

Alisema uongozi wa elimu kwa kushirikiana  na ofisi za mipango katika halmashauri ya wilaya hiyo baadhi ya changamoto zinaweza kutafutiwa ufumbuzi kama kutakuwepo ushirikishaji wa jamii hasa ukusanyaji wa vifaa vinavyopatikana kwa wananchi.

Viongozi mbalimbali wilayani Biharamulo waliohudhuria kilele cha wiki ya elimu katika shule na kata ya Nyamigogo walifanya zoezi la upandaji miti katika shule ya Nyamigogo. 

Na:- Shaaban Ndyamukama –BIHARAMULO.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad