Janga baharini Korea Kusini :-Zaidi ya watu 300 bado hawajapatikana , wawili wamefariki na wengine 164 wameokolewa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, April 16, 2014

Janga baharini Korea Kusini :-Zaidi ya watu 300 bado hawajapatikana , wawili wamefariki na wengine 164 wameokolewa.

Walioshuhudia ajali walisema kuwa walisikia kishindo kikubwa wakati meli hiyo ilipoanza kuzama ambapo Meli ya Korea Kusini iliyokuwa imewabeba zaidi ya abiria mianne ilizama kusini mwa pwani ya nchi hiyo Jumatano (April 16, 2014) asubuhi.


Meli hiyo ilikuwa na watu 460. Zaidi ya miatatu hawajapatikana , wengine 164 wameokolewa na wengine wawili wamethibitishwa kufariki.

Wanafunzi wengi waliokolewa kupitia mashimo yaliyo kando ya meli hiyo huku wengine wakiruka baharini katika jitihada za kuokoa maisha yao.

Walioshuhudia ajali walisema kuwa walisikia kishindo kikubwa wakati meli hiyo ilipoanza kuzama ambapo Meli ya Korea Kusini iliyokuwa imewabeba zaidi ya abiria mianne ilizama kusini mwa pwani ya nchi hiyo Jumatano (April 16, 2014) asubuhi.

"watu walikuwa wakihangaika kukimbilia maeneo ya juu ya meli, lakini ilikuwa vigumu kufanya hivyo kutokana na meli kupinduka."..Bado haijafahamika kilichosababisha…




Watu wawili wameripotiwa kufariki ingawa shughuli ya uokozi ingali inaendelea. Wengine zaidi ya miatatu bado hawajulikani waliko.


Zaidi ya watu miatatu bado hawajapatikana baada ya meli iliyokuwa imewabeba wanafunzi kuzama nchini Korea Kusini.

Awali maafisa walikuwa wamesema kuwa wengi wa abiria waliokuwa katika meli hiyo waliokolewa.

Baadhi ya walionusurika wamekuwa wakielezea hali ilivyokuwa ya kutisha ndani ya meli ilipoanza kusimama kwa kuyumba, ikiegemea upande mmoja na haraka kuanza kuzama.

Bado haijafahamika kilichosababisha kuzama kwa meli hiyo, ambayo kwa kiasi kikubwa iliwabeba wanafunzi wa shule, lakini watu walionusurika katika ajali hiyo wanatoa maelezo sawa kuhusu tukio hilo la kutisha.

Kikosi cha Walinzi wa Pwani ya Korea Kusini kimesema abiria wapatao mia tatu hawajulikani walipo baada ya meli kupinduka na kuzama.

Watu wawili wamefahamika kupoteza maisha na watu mia moja na sitini na wanne wameokolewa.

Wengi wa abiria wa meli hiyo walikuwa wanafunzi wa sekondari wakiwa katika safari ya masomo kuelekea kisiwa cha Jeju, nchini Korea Kusini.

Meli hiyo ilikuwa na watu 460. Zaidi ya miatatu hawajapatikana , wengine 164 wameokolewa na wengine wawili wamethibitishwa kufariki.


Chanzo:-BBC-Swahili.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad