COPA DEL REY 2013/2014:- Real Madrid wainyuka FC Barcelona 2-1 na kutwaa kombe la Mfalme mara 19. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, April 17, 2014

COPA DEL REY 2013/2014:- Real Madrid wainyuka FC Barcelona 2-1 na kutwaa kombe la Mfalme mara 19.


Real Madrid ndiyo mabingwa wa Kombe la Mfalme wa Hispania maarufu kama Copa Del Rey na shujaa ni mchezaji ghali zaidi duniani, Gareth Bale akiwapa Ubingwa huo mara 19 sasa huku FCBarcelona wakilitwaa Kombe hilo mara 26, mara ya mwisho kulitwaa ni 2012.


Klabu ya Real Madrid imetwaa Kombe la Mfalme(Copa del Rey) baada ya kuichapa FC Barcelona mabao 2-1 usiku huu(April 17, 2014) katika Uwanja wa Mestala mjini Valencia, Hispania.

Real Madrid walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 10, mfungaji akiwa ni Angel di Maria akimalizia pasi ya Karim Benzema, lakini Bartra akaisawazishia Barcelona dakika ya 68.

 Bale akishangilia bao lake
dk 85 katika ushindi wa 2-1.
Shukrani kwa Real Madrid usiku wa leo (April 17, 2014) alikuwa ni nyota wa Wales, Gareth Bale aliyefunga bao la ushindi dakika ya 85 na kuwapa Taji hilo Real Madrid.
Barcelona, ambao wameshatwaa Kombe hilo mara 26, mara ya mwisho kulitwaa ni 2012, wakati Real Madrid , ambao wamelitwaa mara 19 sasa, Mwaka Jana 2013 walifungwa Fainali na Atletico Madrid.

Baada ya kunyakua taji la kwanza msimu huu 2013/2014, Real Madrid sasa inaelekeza nguvu zake katika mataji mengine mawili, La Liga na Ligi ya Mabingwa Ulaya ambako imefika hatua ya Nusu Fainali na itamenyana na mabingwa watetezi, Bayern Munich.

Kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Hispania, Real Madrid inachuana na Atletico Madrid walio kileleni na Barcelona walio nafasi ya tatu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad