EPL 2013/2014:-Manchester City kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England sasa kwa fifia baada ya kulazimishwa sare 2-2 na Sunderland. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, April 17, 2014

EPL 2013/2014:-Manchester City kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England sasa kwa fifia baada ya kulazimishwa sare 2-2 na Sunderland.


Matumaini ya Manchester City kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England, yameanza kufifia baada ya kulazimishwa sare ya kufungana mabao 2-2 na Sunderland Uwanja wa Etihad jana April 16,2014 usiku.
MAN CITY wamepata pigo kubwa katika mbio zao za Ubingwa baada ya kutoka Sare ya 2-2 kwenye Mechi ya Ligi Kuu Uingereza waliyocheza kwao Etihad na Timu ya mkiani Sunderland.

Man City walifunga Bao lao la kwanza Dakika ya Pili tu baada ya Alvaro Negredo kuunasa Mpira na kumpasia Sergio Aguero ambae alimsogezea Fernandinho, aliekuwa akiingia ndani ya Boksi, na kupiga shuti la chini na kutinga wavuni.

Lakini Sunderland walicharuka Kipindi cha Pili na Connor Wickham kupiga Bao 2 na kuwafanya waongoze 2-1.

Ilibidi Shuti kali la Samir Nasri liwaokoe Man City zikiwa zimebaki Dakika 2 na kuifanya Mechi iwe Sare ya Bao 2-2 hadi mwisho.

Matokeo haya yamewaacha Man City wakiwa Nafasi ya 3 wakiwa na Pointi 71 na sasa ndoto ya Ubingwa kwao haiko tena mikononi mwao wenyewe.

Kwa Palace, haya ni matokeo ambayo yamehakikisha usalama wao kubaki Ligi Kuu England.

Aidha Ile azma ya Everton ya kumaliza ikiwa 4 Bora imeingia dosari kubwa baada ya kufungwa wakiwa kwao Goodison Park Bao 3-2 na Crystal Palace.

Matokeo haya yamewabakisha Everton nafasi ya 5 nyuma ya Arsenal


Position Team Played Goal Difference Points

1 Liverpool 34 51 77
2 Chelsea 34 42 75
3 Man City 33 54 71
4 Arsenal 34 18 67
5 Everton 34 21 66
6 Tottenham 34 0 60
7 Man Utd 33 18 57
8 Southampton 34 5 48
9 Newcastle 34 -14 46
10 Stoke 34 -10 43
11 Crystal Palace 34 -14 40
12 West Ham 34 -9 37
13 Hull 33 -6 36
14 Aston Villa 33 -14 34
15 Swansea 34 -5 33
16 West Brom 33 -11 33
17 Norwich 34 -27 32
18 Fulham 34 -40 30
19 Cardiff 34 -34 29
20 Sunderland 33 -25 26

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad