BODABODA:-Hatimae Mwili wa Mwendesha pikipiki Bw Idrisa Richard aliyeuwawa na mwili wake kutelekezwa porini,azikwa katika Makaburi ya Nabuhima wilayani Kibondo mkoani Kigoma. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, April 03, 2014

BODABODA:-Hatimae Mwili wa Mwendesha pikipiki Bw Idrisa Richard aliyeuwawa na mwili wake kutelekezwa porini,azikwa katika Makaburi ya Nabuhima wilayani Kibondo mkoani Kigoma.


Muonekano wa wanachama 251 wa Chama cha Bodaboda wilayani Kibondo Mkoani Kigoma kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wilayani humo wakijiandaa kufanya msako na kufanikiwa kumpta mwendesha pikipiki mwenzao Bw Idrisa Richard  akiwa tayari ameuawa na mwili wake kutelekezwa porini-April 02,2014,Marehemu amezikwa leo April 03,2014,katika Makaburi ya Nabuhima wilayani humo.


Hapa waendesha pikipiki wakiwa katika kituo cha mafuta-sheri wakijaza fultank –mafuta wakijiaanda kwenda kumtafuta hapa ni sheri ya Mashaka Stand mpya…Picha Na mdau:- Jerome Dickson-Kibondo



Wanachama 251 wa Chama cha Bodaboda wilayani Kibondo Mkoani Kigoma wakiwa Maeneo ya  Makondeko, Kibondo mjini tayari kwa safari ya kuelekea kuusaka Mwili wa marehemu na hatimae kuupata.


Msafara wa Wanachama  wa Chama cha Bodaboda wilayani Kibondo Mkoani Kigoma ukiwa njiani Kwenda Mazishini katika makaburi ya Nabuhima wilayani humo.


Tunaomba radhi kwa Picha hii(huu ndiyo mwili wa mwendesha pikipiki Bw Idrisa Richard akiwa tayari ameuawa na mwili wake kutelekezwa porini ukiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya wilaya ya Kibondo tayari kwa taratibu za maziko katika makaburi ya Nabuhima wilayani humo.




Msafara wa Wanachama  wa Chama cha Bodaboda wilayani Kibondo Mkoani Kigoma ukiwa njiani Kwenda Mazishini katika makaburi ya Nabuhima wilayani humo.

Wanachama 251 wa Chama cha Bodaboda wilayani Kibondo Mkoani Kigoma kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wamefanya msako na kufanikiwa kumpta mwendesha pikipiki mwenzao Bw Idrisa Richard akiwa tayari ameuawa na mwili wake kutelekezwa porini.

Marehemu amezikwa leo April 03,2014,Katika makaburi ya Nabuhima wilayani humo.

Akizungumza katika eneo la tukio Mwenyekiti wa Chama hicho Bw Elisha Msigwa amesema kuwa Bw Richard ameepotea tangu March 29 ,mwaka huu majira ya saa moja usiku wakati amebeba abiria wawili waliokuwa wakielekea kijiji cha Nyagwijima.

Amesema kuwa wamempata mwenzao huyo akiwa ameuawa kwa kupigwa na kunyongwa na kamba na kisha kuporwa pikipiki yake na vitu vyote alivyokuwa navyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Upelelezi toka Jeshi la Polisi wilayani Kibondo Bw James Ntandu amesema kuwa zoezi la kuwatafuta watuhumiwa wa mauaji hayo linaendelea ambapo ametoa wito kwa wakazi wa wilaya hiyo kutoa taarifa kuhusu watu wanaohisiwa kuhusika ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Habari Na:-Radio Kwizera FM.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad