AJALI:-Watu wawili wamefariki dunia papo hapo na wengine 13 kujeruhiwa baada Basi walilokuwa wakisafiria kupinduka mara kadhaa eneo la Kazilamihunda wilayani Kakonko. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, April 26, 2014

AJALI:-Watu wawili wamefariki dunia papo hapo na wengine 13 kujeruhiwa baada Basi walilokuwa wakisafiria kupinduka mara kadhaa eneo la Kazilamihunda wilayani Kakonko.



Watu wawili wamefariki dunia papo hapo na wengine kumi na tatu kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata pancha ya taili ya nyuma kisha kuanguka  eneo la kazilamihunda wilayani Kakonko mkoani Kigoma, kutokana na mwendo kasi wa gari hilo lililokuwa likitokea Nyakanazi wilayani Biharamulo mkoani Kagera kwenda wilayani Kibondo mkoani Kigoma...Picha Na:-Maktaba yetu.
Jeshi la polisi wilayani Kakonko limesema kuwa waliouwawa ni mwanaume mmoja pamoja na mwanamke mmoja ambao hawakujulikana majina yao mara moja na miili yao iko katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya Kakonko .

Aidha jeshi hilo limebainisha kuwa dereva wa gari hilo Bw.Adrof Sadock ametoroka baada ya kutokea kwa ajali hiyo na mpaka sasa hajulikani aliko .

Baada ya kutokea kwa ajali hiyo basi moja ambalo lilikuwa nyuma ya gari hiyo iliyopata ajali liliwachukua majeruhi wote na kuwakimbiza katika hospitali ya wilaya ya Kibondo kwa matibabu zaidi.

Mganga mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Kibondo,Dr.Frolian Tinuga amekili kupokea majeruhi hao 13 na kwamba hali zao zinaendelea vizuri na wanaendelea na matibabu.

Baadhi ya majeruhi waliokuwemo katika gari hilo wameelezea chanzo cha ajali hiyo wakisema kuwa ni mwendo kasi na kwamba taili la nyuma lilipata pancha hivyo gari liliyumba sana na kusababisha kuanguka na kubinuka mara kadha.

Jeshi la Polisi wilaya ya Kakonko limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba ajali hiyo imehusisha gari aina ya Toyota Hiace lenye namba za usajili T 498 CSM na kwamba upelelezi zaidi wa tukio hilo bado unaendelea.

Habari Na:-James Jovin-Kibondo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad