VPL 2013/2014:-Yanga SC waifua Rhino Rangers Bao 3-0 na kuwakaribi Vinara wa VPL, Ligi Kuu Vodacom, Azam FC kwa kufikisha pointi 43 . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, March 22, 2014

VPL 2013/2014:-Yanga SC waifua Rhino Rangers Bao 3-0 na kuwakaribi Vinara wa VPL, Ligi Kuu Vodacom, Azam FC kwa kufikisha pointi 43 .





Wachezaji wa Yanga SC wakishangilia bao la kwanza lililofungwa na Jerson Tegete ambapo Mabingwa hao watetezi wakiwa huko Tabora waliifunga Rhino Rangers Bao 3-0 na kuwakaribi Vinara wa VPL, Ligi Kuu Vodacom, Azam FC kwa kuwa Yanga SC inafikisha pointi 43 ikiwa katika nafasi ya pili nyuma ya Azam Fc yenye ponti 44 huku timu zote kwa sasa zikiwa zimecheza michezo 20 na kubakisha michezo sita kabla ya kumalizika kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom.

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara timu ya Yanga SC leo March 22,2014 imeibuka na ushindi na mabao 3 - 0 dhidi ya wenyeji timu ya Rhino Rangers katika mchezo uliofanyika jioni ya leo katika dimba la Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora.

Yanga SC ambayo inapigana kuhakikisha inatete Ubingwa wake kwa mara ya pili mfululizo, iliingia uwanjani kwa lengo la kusaka pointi 3 muhimu jambo ambalo wamefanikiwa na kusogea nyuma ya Azam FC kwa tofauti ya pointi moja tu.
Bao za Yanga zilifungwa na Jerry Tegete, Bao 2, na Hussein Javu.

Nako huko Azam Complex, Chamazi, Viunga vya Jiji la Dar es Salaam, Mbeya City iliwachapa Wenyeji wao Bao 2-0 na kujizatiti Nafasi ya 3 kwenye VPL.

Bao zote za Mbeya City zilifungwa na Saidi Kipanga.

Kwa matokeo hayo, Mbeya City wanafikisha pointi 42 katika nafasi ya tatu, pointi moja nyuma ya Yanga wenye pointi 43 baada ya kushinda leo mabao 3-0 mjini Tabora.

Utofauti wa pointi moja unaonesha jinsi ambavyo timu za ligi kuu hasa za juu zinaendelea kupambana kutafuta taji msimu huu.

Ligi hiyo itaendelea kesho Jumapili March 23,2014, kwa mechi nne ambapo Simba itacheza na Coastal Union katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Azam itaoneshana kazi na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Azam Complex. Mechi hizo mbili zitakuwa ‘live’ kupitia Azam Tv.

 Mechi nyingine za kesho Jumapili ni Mgambo Shooting dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, wakati Ruvu Shooting na Ashanti United zitapimana ubavu kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad