![]() |
|
Man City sasa yaungana na Arsenal
kurudi kucheza mechi zao zaLigi kuu soka Nchini Uingereza.
|
Usiku wa Jana March 12,2014, FC
Barcelona na Paris Saint-Germain, zote zimetinga Robo Fainali ya Ligi ya
Mabingwa barani Ulaya UEFA , baada kushinda Mechi zao za Marudiano ya Raundi ya
Mtoano ya Timu 16, wote wakishinda 2-1, kwa FCBarcelona kumchapa Manchester City na PSG kumpiga Bayer Leverkusen.
Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja
wa Camp Nou, mabao ya Barca yalifingwa na Lionel Messi dakika ya 67 na dani
Alves dakika ya 90, wakati bao City lilifungwa na nahodha wake, Vincent Kompany
dakika ya 89.
Man City iliyofungwa 2-0 Uwanja wa
Etihad katika mechi ya kwanza ya hatua ya 16 Bora, ilipata pigo jana dakika ya
78 baada ya mchezaji wake, Pablo Zabaleta kutolewa nje kwa kadi nyekundu.
Katika mchezo mwingine, PSG nayo
ilimalizia vizuri biashara baada ya kuifunga Bayer Leverkusen mabao 2-1 Uwanja
wa Pac de Princes hivyo kufuzu kwa ushindi wa jumla wa 6-1, baada ya awali
kushinda 4-0 ugenini.
MARUDIANO UEFA 2013/2014 MATOKEO.
[Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa
Mechi mbili]
Jumanne Machi 11,2014.
Bayern Munich 1 Arsenal 1 [3-1]
Atletico de Madrid 4 AC Milan 1 [5-2]
UEFA CHAMPIONZ LIGI 2013/2014 MARUDIANO
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya
Kwanza]
[Saa za Bongo]
Jumanne Machi 18,2014.
22:45 Chelsea FC v Galatasaray Spor
Kulübü [1-1]
22:45 Real Madrid CF v Schalke 04 [1-6]
Jumatano Machi 19,2014.
22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit
St. Petersburg [4-2]
22:45 Manchester United v Olympiacos
CFP [0-2]
Hivyo sasa
FC Barcelona, Paris Saint-Germain na Atletico Madrid wanaungana na Mabingwa watetezi Bayern Munich kutinga
hatua ya Robo Fainali ya UEFA .







No comments:
Post a Comment