![]() |
|
Kikosi cha
Timu ya Walimu ama Staff wa Shunga Sekondari kilicho cheza mchezo wa fainali ya kuwania Kombe la Nzoma Cup 2014.
|
![]() |
|
Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Shunga ya
wilayani Ngara wakifurahia ushindi wa Kidato cha pili kuibuka Mabingwa wa Nzoma CUP.
|
Mashindano
ya Nzoma CUP 2014 kwa Walimu na Wanafunzi wa shule ya sekondari Shunga iliyopo wilayani
Ngara mkoani Kagera hatimaye yamemalizika March 11,2014, jioni kwa fainali ya
mchezo wa soka,Hand ball,Netball na Drama.
Katika
mchezo wa fainali katika soka uliochezwa katika uwanja wa shule ya msingi
Murukulazo,uliwakutanisha timu ya Kidato cha Pili dhidi ya Timu ya Walimu ama
Staff na kidato cha Pili kufanikiwa kuwatandika bila huruma Walimu bao 3-1 kwa
bao za Aniseti Musa,Philipo Emanuel na Boaz Richard huku lile la Walimu ambalo
ni lakufutia machozi likifungwa na Mwl.Emanuel Gashaza.
Kufuatia
Ushindi huo wa 3-1, Kidato cha Pili ndio Mabingwa wa Nzoma Cup 2014 na
wameondoka na zawadi ya Mbuzi-mnyama mwenye thamani ya shilingi elfu 50 huku
washindi wa pili wakiwa ni Walimu walioondoka na shilingi elfu 30.
Aidha katika
fainali ya mchezo wa Handball, kidato cha pili waliibuka tena mabingwa kwa
kuwafunga magoli 4-2 kidato cha nne na kuondoka na zawadi ya shilingi elfu 15,katika
mchezo wa netiball, Kidato cha nne wakifanikiwa kuwa Bingwa kwa kuwafunga
Kidato cha tatu goli 17-10 na kuondoka na zawadi ya shilingi elfu 15 huku katika
mchezo wa Drama au Maigizo fainali iliwakutanisha kidato cha kwanza hadi cha nne
na mshindi kuibuka Kidato cha tatu kwa point 258 na kuondoka na zawadi ya Kuku
Jogoo lenye thamani ya shilingi elfu 15.
Nae mdhamini
wa Ligi hiyo ya Nzoma-Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari shunga-Mwl.John
Nzomalarumwe pamoja na kuwapongeza washiriki wote kwa kudumisha nidhamu wakati
wa mashindano hayo ameelezea pia malengo ya mashindano hayo kwa mwaka huu,kuwa
ni kukuza mahusiano baina ya Walimu na Wanafunzi wa shule hiyo.













No comments:
Post a Comment