Katibu
Tawala Msaidizi, Idara ya Miundombinu mkoani Kagera Bw Seif Hussein amesema
serikali inaendelea kufanya ukarabati wa barabara ya Isaka - Rusumo kwa kuwa
imeanza kuharibika kutokana na kujengwa zaidi ya mika 30 iliyopita.
Bw Hussein
amesema hayo March 12,2014, wakati akizungumza na Radio Kwizera wilayani Ngara
mkoani Kagera, kufuatia malalamiko ya wananchi kuhusu kipande cha barabara kutoka Nyakanazi, Biharamulo hadi
Rusumo wanachodai kuwa kero kwa watumiaji wa barabara hiyo.
Amesema kuwa
barabara hiyo hutumika kusafirisha mizigo mizito ndani na nje ya nchi hali
inayosababisha baadhi ya maeneo kuharibika na kwamba barabara hiyo ilitakiwa
kufanyiwa ukarabati wa kudumu baada ya miaka 20 lakini tatizo ni upatikanaji wa
fedha
Hata hivyo Mkuu
wa mkoa wa Kagera ,Kanali mstaafu Fabian Masawe amewataka watumiaji wa barabara
hiyo kuitumia kwa umakini katika kusafirisha abiria na mizigo na kwamba
changamoto za barabara zitapungua baada ya kukamilika kwa ujenzi wa reli ya
kusafirisha mizigo.
Habari Na:-Radio
Kwizera FM.






No comments:
Post a Comment