Tazama Ufunguzi wa Bohari ya Dawa(MSD) kwa mikoa ya Kagera na Geita. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, March 09, 2014

Tazama Ufunguzi wa Bohari ya Dawa(MSD) kwa mikoa ya Kagera na Geita.

Muonekano wa Kituo cha MSD cha Vifaa na Tiba kilichozinduliwa jana March 08,2014,na Naibu Waziri wa afya Dk KEBWE STEPHEN KEBWE, kwa mikoa ya Kagera na Geita, iliyozinduliwa katika eneo la MALAHALA wilayani Muleba mkoani Kagera, itakayohudumia jumla ya vituo 270.

Naibu Waziri wa Afya, STEPHEN KEBWE akikata utepe kuashiria ufunguzi wa kituo hicho cha MSD na katika hatuba yake  Amesema kuwa serikali inasikitika kuona dawa za serikali zinapatikana kwenye vituo vya watu binafsi, huku wananchi wakikosa huduma katika hosptali za serikali, hasa wilaya ya Ngara ikiongoza kwa upotevu wa dawa.
Kaimu mkurugenzi MSD,COSMAS MWAIFYA ambapo alibainisha kuwa Awali, bohari ya Mwanza ilikuwa ikihudumia mikoa 6, halmashauri 37, vituo vya afya na zahanati  elfu moja  na 73.
Mwenyekiti wa Bodi ya bohari ya dawa nchini Tanzania, Profesa ALI MTULIA amesema kituo hiki kitahudumia vituo vyote vya afya mkoani Kagera, na baadhi ya wilaya za Chato, Bukombe na Mbogwe, mkoani Geita.
Picha ya pamoja ya Viongozi mbalimbali waliohudhuria ufunguzi huo wa Kituo cha Vifaa tiba na dawa(MSD) jana March 08,2014 wilayani Muleba mkoani Kagera.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad