Chelsea
wamejichimbia kileleni mwa Ligi Kuu England kwa kuichapa Tottenham Bao 4-0 na
kuongoza Ligi wakiwa Pointi 7 mbele.
Hadi
Mapumziko Mechi hii ilikuwa 0-0.
Kipindi cha
Pili, makosa ya Jan Vertonghen yaliwafungulia Chelsea mvua ya Magoli baada ya
kuteleza akiwa na Mpira na katika jitihada za kuokoa akatoa pasi kwa Samuel
Eto’o ambae alifunga na kusherehekea kama Mtu Mzee ikiwa ni ishara ya kumkejeli
Meneja wake Jose Mourinho ambae Wiki iliyopita alirekodiwa akisema hajui Umri
wa Eto’o na hilo kuibua utata kuhusu Umri wa Straika huyo toka Cameroun.
Bao hilo
lilidumu Dakika 5 tu na kwenye Dkika ya 60 Tottenham walipata mapigo mawili
baada Refa Michael Oliver kuwapa Penati Chelsea na pia kumpa Kadi Nyekundu
Sentahafu wao Younes Kaboul kwa kumchezea Rafu Samuel Eto’o.
Eden Hazard alifunga
Penati hiyo na Chelsea kuongoza 2-0.
Chelsea
waliongeza Bao nyingine, zote kupitia Demba Ba alieingizwa badala ya Eto’o
katika Dakika ya 76, na zote zilitokana na makosa ya Mabeki wa Tottenham huku
moja likifungwa baada Sandro kuteleza na jingine Kichwa cha Kyle Walker kunaswa
kabla kumfikia Kipa Hugo Lloris.
Mabingwa
watetezi wa Uingereza, Manchester United, wakicheza Ugenini huko The Hawthorns,
wameichapa West Bromwich Albion Bao 3-0 na kupanda Nafasi moja na kukamata
Nafasi ya 6.
Bao la
Kwanza la Man United lilifungwa kwa Kichwa na Phil Jones katika Dakika ya 34
kufuatia Frikiki ya Robin van Persie.
Man United
walifunga Bao la Pili kupitia Wayne Rooney kwa Kichwa katika Dakika ya 65
alipounganisha Krosi ya Rafael baada muvu aliyoanzisha mwenyewe na kumhusisha
Juan Mata aliempa Rafael.
Bao la Tatu
lilifungwa na Danny Welbeck baada ya gonga safi ya Pasi 7 zilizomfikia Rooney
aliempenyezea Welbeck na kufunga katika Dakika ya 82.
Mechi
inayofuata kwa Man United ni Jumapili Machi 16 Uwanjani Old Trafford
watakapocheza na Mahasimu wao wa Jadi, Liverpool.
Jumamosi
Machi 8,2014.
West Brom 0
Man United 3
Cardiff 3
Fulham 1
Crystal
Palace 0 Southampton 1
Norwich 1
Stoke 1
Chelsea 4
Tottenham 0
MSIMAMO.
| NA | TIMU | P | GD | PTS |
| 1 | Chelsea | 29 | 34 | 66 |
| 2 | Liverpool | 28 | 38 | 59 |
| 3 | Arsenal | 28 | 24 | 59 |
| 4 | Man City | 26 | 42 | 57 |
| 5 | Tottenham | 29 | 0 | 53 |
| 6 | Man United | 28 | 12 | 48 |
| 7 | Everton | 27 | 11 | 48 |
| 8 | Newcastle | 28 | -2 | 43 |
| 9 | Southampton | 30 | 2 | 42 |
| 10 | West Ham | 28 | -4 | 31 |
| 11 | Aston Villa | 28 | -7 | 31 |
| 12 | Stoke | 29 | -14 | 31 |
| 13 | Hull | 28 | -5 | 30 |
| 14 | Swansea | 28 | -4 | 29 |
| 15 | Norwich | 29 | -22 | 29 |
| 16 | Crystal Palace | 28 | -19 | 27 |
| 17 | West Brom | 28 | -11 | 25 |
| 19 | Cardiff | 29 | -28 | 25 |
| 18 | Sunderland | 26 | -16 | 24 |
| 20 | Fulham | 29 | -36 | 21 |
MECHI
ZIJAZO LIGI KUU.
Jumamosi
Machi 15,2014.
1545 Hull v
Man City
1800 Everton
v Cardiff
1800 Fulham
v Newcastle
1800
Southampton v Norwich
1800 Stoke v
West Ham
1800
Sunderland v Crystal Palace
1800 Swansea
v West Brom
2030 Aston
Villa v Chelsea
Jumapili
Machi 16,2014.
1630 Man
United v Liverpool
1900
Tottenham v Arsenal






No comments:
Post a Comment