![]() |
|
Makamu
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samia Suluhu Hassan akimkumbatia
Mwenyekiti wa Bunge Hilo Samwel Sitta jana March 13,2014,Mjini Dodoma…Picha na
Hassan Silayo MAELEZO.
|
![]() |
|
Mgombea wa
Nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la katiba Bi. Amina Abdallah
akimpongeza Bi. Samia Suluhu Hassan baada ya Kutangazwa kuwa Makamu mweyekiti
wa Bunge Maalum la Katiba.
|
![]() |
|
Mjumbe wa
Bunge Maalum la Katiba Samia Suluhu Hassan akitoa shukrani zake kwa Wajumbe wa
Bunge Maalum la Katiba baada ya Kuteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge hilo.
|
![]() |
|
Katibu wa
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashilila akieleza wajumbe
juu ya utaratibu wa upigaji kura kwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti jana Mjini
Dodoma.
|
![]() |
|
Mgombea wa
Nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la katiba Bi. Amina Abdallah
akinadi Sera zake kwa wajumbe wa Bunge
Maalum la Katiba.
|
![]() |
|
Baadhi ya
Wajumbe wa Bunge Maalum la katiba wakibadilishana Mawazo na Mwenyekiti wa Bunge
Hilo Samwel Sitta(Aliyekaa).
|
Aidha Wajumbe
wa Bunge Maalum la Katiba wamemchagua Bi.Samia Suluhu Hassan kuwa Makamu
Mwenyekiti wa Bunge hilo.
Katika
uchaguzi huo umefanyika Jana March 13,2014, jioni katika ukumbi wa Bunge hilo
Mjini Dodoma, Bi.Suluhu ambaye ni Waziri wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais
anayeshughulikia Muungano, alikuwa akichuana na Bi Amina Abdallah Amour ambaye
ni Mbunge wa viti maalum kupitia CUF.
Akitangaza
matokeo ya uchaguzi, Mwenyekiti wa uchaguzi huo, amesema Bi.Suluhu amepata kura
390 sawa na asilimia 74.6, ambapo Bi .Amour amepata kura 126 ambazo ni sawa na
asilimia 24.1.
Aidha Leo
March 14,2014, asubuhi Katibu na Naibu Katibu wa Bunge hilo wataapishwa kabla
ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti kuapishwa jioni pamoja na wajumbe wa Bunge
hilo.












No comments:
Post a Comment