![]() |
|
Kwa
mujibu wa Wikipedia,Ushirikina ni wazo ambalo halina sababu yenye msingi katika maarifa, au mang'amuzi.
|
Na kwa mujibu wa mtandao wa islamtanzania.org:-Unaelezea kuwa,USHIRIKINA
wa matambiko unatokana na imani kuwa mababu waliofariki wana uwezo wa kuona
matendo ya watoto na wajukuu wao walio hai.
Na inadhaniwa wanapokasirika basi
watoto hupata matatizo ya magonjwa, vifo au mabalaa mengine. Na ili kupoza
hasira zao huko "walikolala" basi hupikwa mapombe na vyakula
vinavyokwenda kumwagwa makaburini au kuliwa na waganga.
Katika
baadhi ya makabila hata viapo huwa ni kuwataja mababu moja kwa moja au kwa
ishara, "alikolala tena!", nikamfufue!, yaani huyo anayesema
anathibitisha akimshuhudisha babu au baba yake aliyekufa kuwa akisemacho ni
sahihi!
Ushirikina wa
matambiko huandamana na mihanga ya pombe au vyakula ili kuilaza mizimu
"iliyochachamalia" koo, familia au jamii fulani.
Mpaka hii
leo bado wako watu wenye imani hizo potofu za kishirikina ambazo huwafanya
wasiweze kuendesha mambo yao kwa namna inayotakikana kwa hofu ya kuwachukiza
mabab.
Kila kabila
lina aina ya matambiko linayofanya kulingana na mila zake. Makabila ya maeneo
ya pwani na morogoro hufanya matambiko yao makaburini na kupeana majina maalum
ya mababu na kuvaa kago (alama) mikononi.
Makabila
mengine hasa ya mikoa ya kaskazini, kati na magharibi hushikamana na mila au
desturi zao za mavazi, ngoma za mashetani, mizuka na vinyamkera vyao kama alama
ya kuwaheshimu na kuwaenzi mababu zao wa kale.
Kwa mfano
wamanyema wana ngoma za mizuka, katika ngoma hizo hupandishwa mashetani kulingana
na tawi husika la kabila hilo kubwa nchini. Yapo mashetani ya kiluwa, kitongo,
kisonge, kibangubangu, kibwari, kibisa nakadhalika.
Wamakonde
nao wanaitakidi kuwa kinachitwadi ndio wanaoua watu kwa hiyo wanadhani kwa
kumdanganya kuwa aliyekufa ndiye mtu wa mwisho wanadhani wanaweza kukiepuka
kifo! Desturi hii hutumika wakati wa kwenda kuzika!
Wanyamwezi
nao wana mashetani yao ya kike na kiume, wamwelu ni shetani la kike huitwa kwa
kupigiwa ngoma inayoitwa migabho, waliopandisha mizuka hiyo hufyonza damu ya
mbuzi aliye hai. Baadhi ya vyakula huwa "mwiko kabisa" kwa wenye
mashetani hayo.
Wapo Waswezi nao kama wanyamwezi mwenendo ni huo huo.
Kauli ya
Qur'an dhidi ya imani hizi za kishirikina ni kwamba Mwenyezi Mungu peke yake
ndiye anayestahiki kuabudiwa kwani Yeye ndiye aliyewaumba watu wote
waliotangulia na waliopo hivi sasa na ndiye pekee aliyewafisha wote
waliotangulia.
Watu wanakatazwa wasiabudie mababu, mizimu wala mizuka kwa
matambiko na mihanga, poza na mengineyo bali wanatakiwa wamuabudie:-
"Mola
wa mbingu na Ardhi na vilivyomo ndani yake, ikiwa mnayo yakini. Hakuna
aabudiwaye kwa haki ila yeye, anahuisha na kufisha, Mola wenu ni Mola wa Wazee
wa mwanzo(44:8).
Eny watu!
Mwabuduni Mola wenu ambaye amekuumbeni nyinyi na wale wa kabla yenu ili mpate
kuokoka. Ambaye amekufanyieni hii ardhi kuwa kama busati na mbingu kuwa kama
paa, na akateremsha maji kutoka mawinguni na kwa hayo akatoa matunda yawe
riziki zenu. Basi msimfanyie Allah washirika na hali nyinyi mnajua(2:21-22).






No comments:
Post a Comment