![]() |
|
Mchezo ukiendelea katika uwanja wa Benaco,kata ya Kasulo wilayani Ngara.
|
![]() |
|
Diwani wa kata ya Kasulo,Mh.Philibert Kiiza mwenye shati la pinki akifatilia mchezo huo wa Ligi ya Makoye 2014,kati ya Benaco FC dhidi ya Bodaboda FC katika kuwania zawadi ya Ngombe -Mnyama.
|
![]() |
|
Aliekanyaga mpira ni Mwenyekiti wa Mashindano hayo ya Makoye,Braitoni Kemikimba na Mratibu wake Nuru Buchwa(kulia wakifatilia moja kati ya mechi za Ligi ya Makoye katika uwanja wa Benaco.
|
![]() |
|
Kikosi cha timu
ya Bodaboda FC kikijadiliana namna ya kucheza na kuwakabili wapinzani wao Benaco FC ambapo katika mchezo huo Bodaboda FC walifungwa bao 1-0.
|
![]() |
|
Kikosi cha timu
ya Benaco FC kilichoifunga Bodaboda FC bao 1-0 katika mchezo wa Ligi ya
Makoye,kikiwa katika Mapumziko ya kipindi cha kwanza ya mchezo wake na Bodaboda FC.
|
![]() |
|
Mashabiki wa timu hizo Bodaboda FC na Benaco FC wakifatilia mchezo huo uliochezwa March 09,2014, katika uwanja wa Benaco.
|
![]() |
| Mashabiki wa timu hizo Bodaboda FC na Benaco FC wakifatilia mchezo huo uliochezwa March 09,2014, katika uwanja wa Benaco. |
Ligi hiyo
ya Makoye 2014,inashirikisha timu 8 kutoka kata ya Kasulo pekee zilizopangwa katika kundi A lenye
timu za Kumunazi Star,Nguvu Kazi FC,Rusumo Sekondari na Kisabule FC huku kundi B likiwa na timu za Watumishi Shooting
Star,Benaco Star,Kago Star na Bodaboda FC ambapo kila kundi litatoa timu mbili
zitakazoingia hatua ya nusu fainali.
Nuru Buchwa ambaye
ni mratibu wa Ligi ya Makoye 2014,amebainisha kuwa Bingwa wa Ligi hiyo ataondoka
na zawadi ya Ng’ombe mwenye thamani ya shilingi Laki 3,Mshindi wa pili fedha
taslimu shilingi 100,000/=,watatu shilingi Elfu 50 ,pamoja na Mchezaji bora na
mfungaji bora kuondoka na shilingi Elfu 10 na Timu yenye nidhamu itaondoka na
Kreti moja la soda.



















No comments:
Post a Comment